• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
Tandahimba District Council
Tandahimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Idara na Vitengo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Kumuona Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoko kwenye Mpango
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Zabuni
    • Kanuni na Taratifbu
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha habari
    • Habari Mpya
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya picha

Wadau Tandahimba wamuunga mkono DC Waryuba mapambano dhidi ya Covid -19

Posted on: May 11th, 2020

Na Kitengo cha Habari na Mawasiliano

Wadau mbalimbali wametoa vifaa tiba  kwa ajili ya mampambano dhidi ya maambukizi ya  ugonjwa wa Covid -19 kuunga mkono jitihada za  Mkuu wa Wilaya ya Tandhaimba Sebastian Waryuba ili wananchi  waendelee kuwa salama


Dc Waryuba  akiwa na Mkurugenzi Mtendaji  Said Msomoka, Katibu Tawala Benaya Kapinga na maafisa wengine wakati wa makabidhiano ya vifaa  nje ya ofisi yake

Wadau ambao wameweza kutoa michango mbalimbali ya vifaa tiba kwa ajili ya mapambano dhidi ya ugonjwa wa Covid -19 ni pamoja na Baraza la madiwani,watumishi,wadau wa elimu ,Chama cha Walimu,Benki ya NMB,Benki ya CRDB na baadhi ya Wafanyabiashara ndani ya Wilaya


Baraza la madiwani wamechangia kila mmoja fedha kwa ajili ya mapambano ya Corona

Akizungumza baada ya Kukabidhi vifaa tiba Afisa Elimu Msingi Hadija Mwinuka amesema kuwa  jitihada hizo zinachukuliwa ili kujikinga na maambukizi ya ugonjwa wa Covid -19 ndani ya Wilaya wananchi waweze kuwa salama na kuendelea na shughuli za maendeleo

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji  ahmada Suleiman akipokea vifaa kutoka kwa Afisa Elimu Msingi Hadija Mwinuka

“Vifaa hivi vimetolewa na Wadau mbalimbali wa elimu ,watumishi wa elimu pamoja na Chama cha Walimu (C.W.T) ikiwa ni jitihada za kuunga mkono agizo la Mkuu wa Wilaya  la kila mtu aweze kuchangia katika mapambano haya ili Wilaya yetu iendelee kuwa salama kwa kujikinga na maambukizi,”amesema Mwinuka


Baadhi ya Watumishi wa Halmashauri ya Tandahimba ambao nao wamechangia fedha katika mapambano ya Covid -19

Naye Meneja wa NMB tawi la Tandahimba Julietha Ndazi  amesema watumishi wameweza kutoa ndoo za kunawia mikono  ili kuunga mkono kauli ya Mkuu wa Wilaya katika mapambano dhidi ya maambukizi ya Covid -19


 

Meneja wa Nmb Tawi la Tandahimba Julietha Ndazi akikabidhi vifaa hivyo

Aidha Meneja wa CRDB tawi la Tandahimba Emmanuel Hitla  amesema  mapambano dhidi ya  maambukizi ya Covid -19 ni ya kila mmoja  hivyo   ili shughuli za maendeleo ziendelee inahitaji wananchi wawe salama kwa kujikinga na virusi vya Corona


 

Meneja wa Crdb Tawi la Tandahimba Emmanuel Hitla akikabidhi vifaa kwa Kaimu Mkurugenzi Ahmada Suleiman

 



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 05, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI November 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MKATABA January 08, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MKIMBIZA MWENGE KIWILAYA March 30, 2024
  • Soma

Habari mpya

  • DC MNTENJELE AKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO SEKTA YA ELIMU

    June 25, 2025
  • DED MWANZALIMA ATEMBELEA MIRADI YA ELIMU

    June 21, 2025
  • TANDAHIMBA YAPATA HATI SAFI MARA YA TANO MFULULIZO.

    June 17, 2025
  • WAZIRI SIMBACHAWENE AMPONGEZA MKURUGENZI WA TANDAHIMBA NA MADIWANI KWA KUFANYA ZIARA YA MAFUNZO SIMIYU.

    June 11, 2025
  • Soma

Video

MKUU WA WILAYA YA TANDAHIMBA PAMOJA NA MKURUGENZI WASHIRIKI UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAHEHA
Video nyingin

Kurasa za karibu

  • Ijue Tandahimba.

Viungio vinavyousiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • President's Official Website
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya sehemu

Tandahimba District Council

Wasiliana Nasi

    TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA

    Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA

    Simu: +25523 2410030

    Simu:

    Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa