• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
Tandahimba District Council
Tandahimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Idara na Vitengo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Kumuona Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoko kwenye Mpango
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Zabuni
    • Kanuni na Taratifbu
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha habari
    • Habari Mpya
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya picha

Huduma za Elimu

Education Services

ELIMU YA AWALI NA MSINGI

Kwa upande wa elimu ya msingi, Wilaya ina jumla ya shule 127. Shule zina jumla ya wanafunzi 62058 . Kati ya hawa wavulana ni 30619 na wasichana ni 31439. Aidha idadi ya Wanafunzi wa Awali jumla ni 7906,Wavulana 4023 naWasichana 3883 na vituo vya walimu 5 ambavyo niTandahimba,Mchichira,Mihambwe,Chikongola na Luagala.Jumla ya mahitaji ya WalimuKatika Halmashauri yetu ni 1856 kwa sasa kuna jumla ya Walimu 965  ambapoWanaume 666 na Wanawake 299 kuna upungufu wa Walimu 894.Waratibu kata wapo 32 ambapo Wanaume 26 na Wanawake 6

Uandikishaji katika shule za Awali na msingi kwa mwaka 2022 nikama ifuatavyo:-

Darasa la Awali  Jumla ya wanafunzi 7906 sawa na asilimia 98 waliandikishwaambapo Wavulana 4023  na Wasichana 3883

Darasa la kwanza Jumla ya Wanafunzi 7428 sawa na asilimia109 waliandikishwa ambapo Wavulana 3717 na Wasichana 3711 

Hali ya Ufaulu ya Darasa la saba katika Halmashauri ya Tandahimbakwa mwaka 2021 waliofanya Mtihaniwa darasa la saba Jumlani 6373,Wavulana 3073 na Wasichana 3300  waliofaulu 4760 sawana asilimia 75

Hali ya Ufaulu wa upimaji wa Kitaifa wa Darasa la nne mwaka 2021,Waliofanya Mtihani 7061  waliofaulu 6655 sawa naasilimia 94.3


Elimu ya Watu Wazima na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi (EWW&ENMRA)

Wilaya yetu imekuwa na mipango madhubuti ya kumpatia mtu mzimaelimu kupitia programu mbalimbali za Elimu ya watu Wazima kama ifuatavyo:Mpango wa Elimu Kwa Walioikosa (MEMKWA), tuna madarasa ya wanafunzi wa MEMKWA katik shule za msingi za Matogoro, Jangwani, Mnyawa, Tandahimba, Ruvuma,Chikongola, na  Mitondi A. Kisomo chenye manufaa (KCM) tuna madarasakwenye vijiji vya Lienje, Pemba, Majengo, Namdowola, Mitondi A na Mitondi B, naMpango wa Uwiano Kati ya Elimu ya Watu Wazima na Jamii (MUKEJA) na Kisomo ChaKujiendeleza (KCK). Changamoto zinazoikabili wilaya katika utoaji wa elimu nipamoja na mwamko mdogo wa kieliemu katika jamii, upungufu wa madarasa ya elimuya watu wazima, walimu wenye sifa, upungufu wa nyumba za walimu, ofisi na vifaavya kufundishia na utoro. Baadhi ya malengo katika kipindi hiki cha mpango nipamoja na kuongeza idadi hiyo ya madarasa katika kila shule ya msingi, kuongezaidadi ya watoto, vijana na watu wazima wanaosajiliwa kuhudhuria masomo namafunzo kwenda shule kutoka 80% hadi 95% ya wanaoandikishwa, kupunguza utoroshuleni, kuongeza idadi ya madarasa yanayojengwa, nyumba za walimu, ukarabatiwa majengo, ujenzi wa matundu ya vyoo na kuboresha Kituo cha Ufundi StadiMatogoro ili kiweze kusajili vijana wengi zaidi.

Historia ya Elimu ya Watu Wazima inaanziawakati wa ukoloni, miaka ya mwanzo baada ya uhuru, mara baada ya kutangazwa kwaazimio la Arusha linalohusu siasa ya ujamaa na kujitegemea, wakati wautekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Kurekebisha Uchumi (Tanzania EconomicStructural Adjustment Programme) na wakati wa maandalizi na utekelezaji waMpango wa Maendeleo wa Sekta ya Elimu (Education Sector Development Programme).Sababu za kuanzisha na kuendeleza mipango ya Elimu ya Watu Wazima zinatokana nanyakati na malengo yake.

Tafsiri ya Elimu ya Watu Wazima (EWW) na ile ya Elimu Nje ya MfumoRasmi (ENMR) zinatofautiana. Hizi ni sekta ndogo mbili kati ya tatu zilizomokwenye mfumo wa elimu ambazo zote lengo lake kuu ni kutoa maarifa, ujuzi nakujenga muelekeo katika haiba na mwenendo wa mtu au jamii.

Elimu ya watu wazima hujumuisha maarifa na ujuzi ambao hutolewakwa watu wazima ili kuinua ubora wa maisha yao kutokana na shughuli au kaziwanazofanya katika mazingira yao. EWW hujumuisha mafunzo ya stadi za kusoma,kuandika na kuhesabu (KISOMO chenye manufaa na KISOMO cha kujiendeleza) aumasomo ya kujiendeleza katika maswala ya kilimo, ufugaji, afya malezi ya watoto,mazingira, ufundi, uchimbaji madini, uvuvi na maarifa mengineyo na ujuzitofauti tofauti. Mafunzo ya mtaala mpya katika KISOMO cha kujiendeleza (mafunzoya kilimo na mifugo, sayansi kimu, afya na lishe na ufundi) ni sehemu ya EWW.Aidha, kuna mafunzo mengine kwa watu wazima ya taaluma; mfano mafunzo ya cheti(Astashahada), Stashahada (Diploma) na Shahada, yanayotolewa na taasisimbalimbali kama vile Elimu ya Watu Wazima na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

Elimu Nje ya Mfumo Rasmi ni maarifa na ujuzi unaotolewa bila kujali rika la washiriki na hutolewa Nje ya Mfumo Rasmi wa shule (watoto,vijana na watu wazima). Mfumo huu haufuati muundo wa madarasa kama vile elimuya awali miaka miwili, elimu ya msingi miaka saba, elimu ya sekondari miaka 4.'A' level miaka 2, chuo kikuu miaka 3-6. Hivyo ENMR ni nyumbufu katika muundo(Structure), mitaala (curriculum), walimu, vifaa vya kufundisha (Teachingmaterials), muda wa kusoma (flexible time), na tathmini (Assessment). Mifano yaENMR ni pamoja na Mpango wa Elimu ya Msingi kwa Walioikosa (MEMKWA), Mpango WaElimu ya Sekondari kwa Walioikosa (MESKWA), Elimu Masafa na Ana kwa Ana (openand distance Learning). Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima na Chuo Kikuu Huria –Tanzania ni mifano ya taasisi zinazotoa elimu nje ya mfumo rasmi. Kwa ufupi EWWna ENMR ni mifumo ya Elimu ambayo inasisitiza kuwa Elimu haina mwisho au kuishini kujifunza (lifelong learning). Mifumo hiyo inaimarisha mchakato wa kupatamaarifa, ujuzi kazi ambao unasaidia ubunifu na kupata mwelekeo ulio sahihikatika maisha ya mtu.

ELIMU YA SEKONDARI

  • Utangulizi

Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba ina shule za sekondari 28 ambazo zinajumla ya wanafunzi 11,242 wakiwemo wavulana 5,228 na wasichana 6,014. Shule ya sekondari Tandahimba ina wanafunzi 190 wavulana  wanaosoma  kidato cha tano na sita (A-level). Pia, shule za sekondari za Halmashauri ya Tandahimba ina walimu 408 wanafundisha masomo ya sayansi, sanaa na biashara.

1.2 Hali ya miundombinu

Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba inafanya juhudi kubwa katika kujenga na kukarabati miundombinu katika shule za sekondari. Hali ya miundombinu kwa sasa ipo kama ifuatavyo;

Jedwali 1: Hali ya miundombinu

Na

Aina ya Miundombinu

Mahitaji

Yaliyopo

Upungufu

1

Madarasa

334

388

0

2

Maabara

54

53

1

3

Nyumba za walimu

439

111

328

4

Matundu ya vyoo vya wavulana

214

147

67

5

Matundu ya vyoo vya wasichana

312

150

162

  •  Mahitaji ya Walimu

Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba yenye shule 28 na wanafunzi 11,242 wa kidato cha kwanza hadi sita inauhitaji wa walimu 489 wakiwemo walimu 67 wa masomo ya sayansi, walimu watatu (3) wa masomo ya biashara, walimu 338 wa sanaa kama inavyoonekana katika jedwali 1.3 

Jedwali 2:  Mahitaji ya Walimu

 

Mahitaji

Waliopo

Upungufu

Walimu wa Sayansi

211

67

144

Walimu wa Biashara

14

3

11

Walimu wa Sanaa

264

338

0

Jumla kuu

489

408

155

1.4 Maendeleo ya Elimu Sekondari 

1.4.1 Ujenzi wa shule mpya 

Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba inaendelea kutekeleza Sera ya Elimu na Ufundi 2014 kwa kufanya upanuzi wa fursa za elimu kwa kujenga shule za sekondari mpya tatu kwa ajili ya mapokezi ya wanafunzi wa kidato cha kwanza mwaka 2023 . Shule hizo zinajengwa katika Kata za Litehu, Kwanyama, na Mndumbwe. Ujenzi wa shule za sekondari Mndumbwe na Kwanyama umetekelezwa kwa nguvu za wananchi na Halmashauri na shule ya Litehu imejengwa kupitia mradi wa SEQUIP (Secondary Education Quality Improvement Programme). Katika mwaka wa fedha 2022/2023 serikali imetoa fedha 120,000,000 kati ya Tsh. 200,000,000 kutekeleza ujenzi wa madara matatu(3) katika shule ya mpya ya sekondari Kwanyama na madarasa matatu (3) katika shule mpya ya sekondari ya Mndumbwe.

Jedwali 3: Ujenzi wa shule mpya

Jina la shule

Idadi ya madarasa

Idadi ya wanafunzi (Nafasi zilizopo)

Hatua iliyofikiwa

Mndumbwe

9

80

Kazi ya ukamilishaji unaendelea
Kwanyama

7

80

Kazi ya ukamilishaji unaendelea
Litehu

14

80

Kazi ya ukamilishaji unaendelea

1.4.2 Utekelezaji wa ujenzi wa madarasa 

Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba inaendelea na utekelezaji wa ujenzi wa  madarasa kumi (10) kwa gharama ya Tsh. 200,000,000/= kutoka serikali kuu kwa ajili ya kuwapokea wanafunzi wa kidato cha kwanza mwaka 2023. Madarasa haya yanajengwa katika sekondari za Tandahimba (madarasa 4), sekondari ya Kwanyama (madarasa 3) na sekondari ya Mndumbwe (Madarasa 3) madarasa yote yapo katika hatua ya ukamilishaji.

1.4.3 Mfuko wa elimu

Kupitia Mfuko wa Elimu idara ya elimu imepata fedha kiasi cha shilingi 132,600,000/= ambazo zitatumika kutekeleza miradi ya ujenzi katika shule saba za sekondari kama ifuatavyo,  

Jedwali 4: Miradi iliyotekelezwa kupitia mfuko wa elimu

NA

JINA LA SHULE YA SEKONDARI

FEDHA TOLEWA 

 

MRADI

HATUA ZILIZOFIKIWA

1

Mchichira
             10,000,000
Ukarabati wa vyumba viwili (2) vya madarasa
Maandalizi ya ujenzi

2

Chaume
               6,300,000
Ukarabati wa vyumba viwili (2) vya madarasa
Maandalizi ya ujenzi

3

Mkwiti
               6,300,000
Ukarabati wa vyumba viwili (2) vya madarasa
Maandalizi ya ujenzi

4

Kitama
             59,000,000
Ukamilishaji wa bweni la wasichana
Maandalizi ya ujenzi

5

Kitama
               5,000,000
Kutengeneza meza na viti
Maandalizi ya ujenzi

6

Kitama
             16,000,000
Kukarabati hosteli
Maandalizi ya ujenzi

7

Mnyawa
             30,000,000
Ujenzi wa nyumba ya walimu
Maandalizi ya ujenzi

JUMLA

          132,600,000 


 



Jedwali: 1.4.2.1 MATOKEO YA MITIHANI YA KIDATO CHA NNE TOKA 2019 HADI 2021

 

 

MWAKA

 

WALIOSAJILIWA

 

WALIOFANYA

 

DARAJA I

 

DARAJA II

 

 

DARAJA III

 

DARAJA IV

 

DARAJA 0

 

WV

 

WS

 

JML

 

WV

 

WS

 

JML

 

WV

 

WS

 

JML

 

WV

 

WS

 

JML

 

WV

 

WS

 

JML

 

WV

 

WS

 

JML

 

WV

 

WS

 

JML

2019

738

940

1678

727

917

1644

63

5

68

101

37

138

199

120

319

475

989

1464

66

230

296

2020

669

871

1540

660

828

1488

67

13

80

106

44

150

194

152

346

535

1067

1612

67

168

235

2021

795

1027

1822

787

1001

1788

43

16

59

103

33

136

169

94

263

640

1028

1668

128

283

411

 

 

Jedwali: 1.4.2.2 MATOKEO YA UPIMAJI KIDATO CHA NNE TOKA 2019 HADI 2021

 

 

MWAKA

 

WALIOSAJILIWA

 

WALIOFANYA

 

DARAJA I

 

DARAJA II

 

 

DARAJA III

 

DARAJA IV

 

DARAJA O

 

WV

 

WS

 

JML

 

WV

 

WS

 

JML

 

WV

 

WS

 

JML

 

WV

 

WS

 

JML

 

WV

 

WS

 

JML

 

WV

 

WS

 

JML

 

WV

 

WS

 

JML

2019

994
1483
2481
904
1381
2285

9

0

9

83

22

105

123

52

175

408

579

987

104

264

368

2020

1054
1534
2588
973
1454
2427

24

6

30

111

37

148

160

80

240

333

606

939

41

90

131

2021

1205
1583
2788
1082
1471
2553

28

0

28

35

98

133

79

193

272

708

404

1112

66

177

243

 

  . 

Elimu ya Ufundi Stadi

Wilaya ina Vituo viwili vya Elimu ya Ufundi Stadi; Matogoro na Luagala Mission. Vijana wanaomaliza darasa la VII wanayo fursa ya kujiunga na vituo hivi vya ufundi stadi vilivyopo Matogoro na Luagala Mission na kupata mafunzo ya ufundi wa useremala, uashi na sayansi kimu. Katika  kipindi cha miaka ya hivi karibuni idadi ya wanafunzi wanaohitimu mafunzo ya ufundi stadi imepungua kutoka wanafunzi 41 mwaka 2016 hadi wanafunzi 25 mwaka 2020. Kuna changamoto anuai zinazosababisha hali hiyo ikiwemo upungufu/ukosefu wa vifaa/zana za kufundishia na kujifunzia, rasilimali fedha na walimu wenye ujuzi na taaluma katika fani zinazofundishwa.

Kutokana na mahitaji makubwa ya Elimu ya Ufundi Stadi kwa vijana na watu wazima hususani wanaomaliza darasa la VII, kidato cha IV na VI hata vyuo vikuu, Halmashauri ina mpango wa kufanya maboresho makubwa katika Kituo cha Ufundi Stadi Matogoro ili kiweze kufundisha fani za useremala, uashi, sayansi kimu, uhunzi, umeme na kompyuta. Lengo ni kuwawezesha vijana na watu wazima wengi wapate maarifa, stadi na ujuzi utakaowawezesha kuajiriwa au kujiajiri. Halmashauri tunaamini njia mojawapo ya kupunguza tatizo la ajira kwa wananchi wetu ni kuwawezesha kupata ujuzi na maarifa kupitia elimu ya ufundi stadi.



Matangazo

  • TANGAZO LA WALIOFAULU USAILI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. January 15, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI November 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MKATABA January 08, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MKIMBIZA MWENGE KIWILAYA March 30, 2024
  • Soma

Habari mpya

  • DC MNTENJELE AKABIDHI VISHIKWAMBI KWA MAAFISA UGANI TANDAHIMBA

    February 18, 2025
  • KU WILAYA YA TANDAHIMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU MWAKA 2025

    February 17, 2025
  • Vipaumbele Mahususi vya Bajeti ya 2025/2026 Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba.

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI TANDAHIMBA LAPITISHA MAKISIO YA MPANGO NA BAJETI YA TSH .BIL.40.2 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026.

    February 13, 2025
  • Soma

Video

MKUU WA WILAYA YA TANDAHIMBA PAMOJA NA MKURUGENZI WASHIRIKI UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAHEHA
Video nyingin

Kurasa za karibu

  • Ijue Tandahimba.

Viungio vinavyousiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • President's Official Website
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya sehemu

Tandahimba District Council

Wasiliana Nasi

    TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA

    Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA

    Simu: +25523 2410030

    Simu:

    Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa