• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
Tandahimba District Council
Tandahimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Idara na Vitengo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Kumuona Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoko kwenye Mpango
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Zabuni
    • Kanuni na Taratifbu
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha habari
    • Habari Mpya
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya picha

Huduma za afya

TAARIFA YA IDARA YA AFYA JULAI  - SEPTEMBA 2022

Halmashauri ina jumla ya vituo 46 vya kutolea huduma za afya. Katika vituo hivyo kuna Hospitali 1 inayomilikiwa na serikali, vituo vya afya 3 kimoja kati ya vituo hivyo kinamilikiwa na shirika la dini la Roman Catholic na  vituo 2 vinamilikiwa na  serikali.Pia  kuna zahanati 42, zahanati 32 kati ya hizo  zinamilikiwa na serikali na 10 zinamilikiwa na  watu binafsi.Pia kuna maduka ya dawa muhimu 105 yanayomilikiwa na watu binafsi na phamasi 2 za watu binafsi.

Hali ya dawa

Hali ya upatikanaji wa dawa katika vituo vya kutolea huduma za afya vinavyomilikiwa na serikali inaridhisha.Uwepo wa dawa (Tracer Medicine) ni 97%, Halmashauri  imekuwa ikihakikisha kuwa kila kituo kinakuwa na dawa za ( Oxtocin & Magnesium Sulphate ) kwa ajili ya kuzibiti kifafa cha mimba kwa wajawazito na utokwaji wa damu kwa wingi baada ya kujifungua. Vituo vyote vinapatiwa dawa, vitendanishi vya maabara na vifaa tiba  kupitia vyanzo mbalimbali vya fedha ikiwepo fedha ya ruzuku za madawa zinazotumwa bohari ya madawa (MSD), fedha za uchangiaji huduma za afya na Bima ya Afya (NHIF), CHF na fedha za mfuko wa pamoja wa wafadhili ( Basket Fund)..

 

Mapokezi ya Vifaa Tiba

  1. Halmashauri kupitia idara ya Afya imepokea mashine ya kisasa ya X-ray (Digital Machine) kutoka OR – TAMISEMI inatarajiwa kufungwa hospitali ya wilaya, ukarabati wa jengo la X-ray unaendelea ili mashine hii mpya iweze kusimikwa kwani mashine iliyokuwepo ni (analogy) imepitwa na wakati hata vifaa vyake havipatikani”Films
  2. Pia tumepokea kitanda na taa maalum ya chumba cha upasuaji katika kituo cha Afya Maheha

 

Ujenzi wa tanuri la kisasa la kuchomea taka Hospitali ya Wilaya

Halmashauri kupitia Wizara ya Afya imepata msaada wa ujenzi wa Tanuri la kisasa ambalo litakuwa linatumia umeme katika uchomaji wa takataka. Ujenzi wa tanuri hilo unaendelea katika Hospitali ya Wilaya’HIGH TECH INCINERATOR’

 

Hali ya watumishi

Idara ya Afya inakabiliwa na upungufu wa watumishi wa kada mbalimbali kwa kiwango cha asilimia 62.8% wanaohitajika ni 780 na waliopo ni 290 ambao ni sawa na asilimia 37.18%. Idara ya Afya imepokea jumla ya watumishi wapya 4 wengine kuziba pengo la watumishi wawili ambao hawakuripoti mwanzo

Mapambano dhidi ya ukimwi

Kwa sasa  maambukizi ya ukimwi ni 1.6%. Katika kuthibiti na kuzuia maambukizi mapya Halmashauri inaendelea  kutoa huduma za ushauri nasaha na upimaji wa VVU. Aidha Halmashauri bado inaendelea  kutoa  elimu kwa wananchi jinsi ya kujikinga na maambukizi ya VVU kwa wananchi wasio na VVU pamoja na kutoa  elimu ya kujikinga na maabukizi mapya kwa wananchi wanaoishi na VVU pamoja na kutoa tiba kinga kwa makundi hatarishi ikiwemo wanawake wanaojiuza na watu wanaoishi na wenzi walioathirika. Pia halmashauri inatoa dawa na ushauri kwa ajili ya kuzuia maambukizi kutoka kwa mama mjamzito kwenda kwa mtoto. Halmashauri ina jumla ya vituo 13 vinavyotoa huduma za CTC ikiwemo ushauri nasaha na upimaji wa VVU, upimaji wa kinga za mwili (CD 4).Katika kipindi cha Julai -Septemba 2022 jumla ya watu 4698  walipima VVU na kati yao waliokutwa na maambukizi ni 97 ambao ni sawa na asilimia 2.1%.

Taarifa ya upimaji na ushauri nasaha wa VVU

CHINI YA MIAKA 14
WALIOKUTWA NA MAAMBUKIZI
JUU YA MIAKA 14
WALIOKUTWA NA MAAMBUKIZI
JUMLA WALIOPIMA
ME
KE
ME
KE
JUMLA
JUMLA WALIOPIMA
ME
KE
ME
KE
JUMLA
32
15
17
1
2
3
4666
2190
2476
52
42
 
94














 

Mapambano dhidi ya Malaria.

Katika kupambana na ugonjwa wa malaria idara ya afya inaendelea kutoa elimu kwa wananchi jinsi ya kujikinga na maambukizi kwa njia mbalimbali ikiwemo usafi wa mazingira na matumizi sahihi ya vyandarua vyenye viatilifu. Jumla ya waliopima Malaria walikuwa 36,581 ambapo wanaume walikuwa 15,565 na wanawake walikuwa 21,016, waliokutwa na maambukizi ya malaria walikuwa 18,470 kati yao wanaume walikuwa 8,103 na wanawake walikuwa 10,367 sawa na asilimia 50%. Wajawazito waliopewa vyandarua walikuwa 1,908 na watoto waliopewa vyandarua walikuwa 2,406 .

Huduma za maabara

Katika kipindi cha Julai -Septemba jumla ya chupa 564sawa na 87% za damu zilikusanywa kwa ajili ya wagonjwa wanaohitaji damu ikiwemo wajawazito, watoto na wagonjwa wengine wenye uhitaji wa damu.Pia huduma zingine za upimaji wa vipimo mbalimbali zilitotolewa ikiwemo magonjwa ya kuambukiza na ya siyo ya kuambukiza.

mengineyo.

Huduma za chanjo

Katika kupambana na magonjwa yanayozuilika kwa chanjo Halmashauri imekuwa ikiendelea kutoa huduma za chanjo kwa ajili ya kukinga watoto dhidi ya magonjwa ya pepopunda, kifaduro, dondakoo, kichomi, kifua kikuu, kupooza na kuharisha. Lengo la chanjo Kitaifa ni kuwachanja watoto zaidi ya asilimia 90% katika robo hii huduma za chanjo zilizotolewa ni kama ifuatavyo.

  1. BoPV               4,231 = 89%
  2. MRi1               4,981   = 105%
  3. MRi2               2,502   = 53%
  4. BCG                5,336   =101%
  5. PCV1              4,774   =101%
  6. PCV3              4,289   =90%
  7. DPT                 4,209   =89%
  8. Rota1              3,667   = 85%
  9. Rota2              4,044   = 77%

Kampeni ya Chanjo ya Polio awamu ya pili

Tarehe 1-4/9/2022 kulifanyika kampeni ya chanjo ya Polio awamu ya pili kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano lengo la Halmashauri ilikuwa ni kuchanja watoto 40,607 lakini ilifanikiwa kuchanja 46,249 sawa na asilimia 113%.

Chanjo ya Uviko

Katika kipindi cha Julai hadi September jumla ya watu  67,536 walipatiwa chanjo ya Uviko kati yao wanaume 26,338 na wanawake 41,198.

Hali ya mfuko wa afya ya jamii. (CHF)

Julai – Septemba 2022 ,tumefanikiwa kusajili kaya 99 zilizojiunga na iCHF zenye wanachama 495  mpaka sasa kuna jumla ya kaya 1,378 zilizojiunga na iCHF zenye wategemezi 6,627 ambazo ni  sawa na 4 % lengo ni kuandikisha 32,532 kati ya kaya 65,064 ambazo ni sawa na asilimia 50% ya kaya zisizotumia Bima ya Afya (NHIF).

 

Huduma Za Lishe

Shughuli za lishe zilizofanyika kwa robo hii ya kwanza ni udhibiti wa matatizo makuu ya Lishe nchini ambayo ni upungufu wa madini joto, utoaji wa nyongeza ya Vitamini A, na utambuzi wa watoto utapiamlo pamoja na matibabu ya utapiamlo mkali.

Katika robo hii tumefanikiwa kutoa elimu ya ulishaji watoto wachanga na wadogo kupitia vituo vyetu vya kutolea huduma za Afya ngazi ya jamii. Jumla ya wazazi/walezi 14,162 waliweza kufikiwa ikiwa ni mapambano endelevu dhidi ya udumavu. Aidha elimu juu ya Lishe bora kwa watu wote inaendelea kutolewa katika vituo vyote vya kutolea huduma za Afya.

Jumla ya walengwa wa Vitamini A kwa robo hii walikuwa 3,570 na waliopatiwa Vitamini A ni 3,932 sawa na 110%.

Walengwa wa utapiamlo mkali ni  kwa robo hii ni  45. Jumla ya watoto waliobainika ni 28 waliopatiwa matibabu na kupona ni 27. Mtoto 1 anaendelea na matibabu.

Ukaguzi wa chumvi zenye madini joto ulifanyika  katika maduka ya Tandahimba na Kitama, jumla ya sampuli 23 zilipimwa kutoka katika maduka madogo, sampuli  18 (78%) zilikua na madini joto na sampuli 5(22%) hazikuwa na madini joto.

Aidha tulipima chumvi kwa ngazi ya kaya kwa kutumia wanafunzi wa shule  ya msingi Matogoro. Jumla ya sampuli 176 zilipimwa. Sampuli 158 (90%) Zilikua na madini joto ya kutosha na sampuli 18(10%) hazikuwa na madini joto kabisa.

Maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji dunia kuanzia tarehe 1-7/08/2022 ambapo elimu ya ulishaji wa watoto wachanga na wadogo ilitolewa kupitia vituo vyote vya kutolea huduma za Afya na Wahudumu wa Afya ngazi ya Jamii.Jumla ya wazazi/walezi 9,196 (70 %).

 

 Imeandaliwa na

Dr.Grace Paul

Kny:Mkurugenzi Mtendaji (W)


Matangazo

  • TANGAZO LA WALIOFAULU USAILI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. January 15, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI November 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MKATABA January 08, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MKIMBIZA MWENGE KIWILAYA March 30, 2024
  • Soma

Habari mpya

  • DC MNTENJELE AKABIDHI VISHIKWAMBI KWA MAAFISA UGANI TANDAHIMBA

    February 18, 2025
  • KU WILAYA YA TANDAHIMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU MWAKA 2025

    February 17, 2025
  • Vipaumbele Mahususi vya Bajeti ya 2025/2026 Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba.

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI TANDAHIMBA LAPITISHA MAKISIO YA MPANGO NA BAJETI YA TSH .BIL.40.2 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026.

    February 13, 2025
  • Soma

Video

MKUU WA WILAYA YA TANDAHIMBA PAMOJA NA MKURUGENZI WASHIRIKI UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAHEHA
Video nyingin

Kurasa za karibu

  • Ijue Tandahimba.

Viungio vinavyousiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • President's Official Website
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya sehemu

Tandahimba District Council

Wasiliana Nasi

    TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA

    Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA

    Simu: +25523 2410030

    Simu:

    Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa