• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
Tandahimba District Council
Tandahimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Idara na Vitengo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Kumuona Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoko kwenye Mpango
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Zabuni
    • Kanuni na Taratifbu
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha habari
    • Habari Mpya
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya picha

Viwanda vidogo vya kukamua mafuta ya alizeti kujengwa Litehu,Mahuta na Namikupa

Posted on: February 1st, 2022

Na  Kitengo cha Habari na Mawasiliano

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba  ndugu Mussa Gama amewaomba wakulima kuchangamkia mbegu  za ufuta na alizeti  zinazotolewa bure  na Halmashauri  kupitia Idara ya kilimo

Mkurugenzi Mtendaji ndugu Mussa Gama akitoa majibu kwa madiwani

Amesema kuwa Halmashauri ya Tandahimba inatarajia kuwekeza viwanda vidogo vitatu  vya kukamua mafuta ya alizeti katika Tarafa tatu ya Litehu,Namikupa na Mahuta ambapo zinatasaidia mkulima kuuza  zao hilo kwa urahisi

Wakuu wa Idara na vitengo walioshiriki kwenye kikao cha baraza la madiwani

Ameyasema hayo  kwenye kikao cha kawaida cha baraza la madiwani baada ya kusoma taarifa yake na Mhe.Hamza Balakali Diwani wa kata ya kwanyama kuhoji uhakika wa  soko kwa wakulima ambao zao la alizeti katika Wilaya yao ni jipya kibiashara

Waheshimiwa madiwani wakiwa kwenye kikao katika ukumbi wa mikutano

“Halmashauri tunaendelea kusambaza mbegu za alizeti kilo 300 na ufuta kilo 3000,niwaombe madiwani wahimizeni wananchi kulima na mazao mbadala ya kibiashara kama alizeti na ufuta,Halmashauri tunatarajia kuwekeza viwanda vidogo  vitatu vya kukamua mafuta ya alizeti kwaiyo soko litakuwepo hapa hapa Tandahimba,”amesema Mkurugenzi

Aidha akitoa muelekeo wa  bei za viuatilifu katika maandalizi ya msimu ujao amesema utaratibu ambao umeandaliwa ni mkulima kuchangia asilimia 50 ya bei ya sokoni na serikali asilimia 50 ambapo utaratibu utaratibiwa na  chama kikuu kwa kushirikiana na vyama vya msingi

Naye Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Mhe. Kanali Patrick Sawala amewasistiza madiwani kuhakikisha katika maeneo yao wananfunzi waliochaguliwa kidato cha kwanza wanakwenda shule lakini pia wananfunzi wanaotakiwa kuanza darasa la kwanza na awali wanapelekwa shule kwa wakati

Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Mhe.Kanali Patrick Sawala akisistiza jambo kwa madiwani

“Sioni sababu ya wanafunzi hadi leo kutoripoti shuleni,nawaomba madiwani mkalisimamie hili katika maeneo yenu,mwanafunzi ambaye hataripoti shule hatua kali tutamchukulia mzazi wake,katika hili tutakua wakali kwasababu Mhe.Rais amejenga miundombinu mizuri,hata kama mwanafunzi hana sare za shule aripoti shule mengine yatafuata,”amesema Dc Sawala

Waheshimiwa madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

Katika kikao hicho cha siku mbili madiwani waliweza kuwasilisha taarifa zao za maendeleo ya  kwenye kata zao sambamba na kumshukuru Mhe.Samia Suluhu Hassan kwa ujenzi wa vyumba 88 vya madarasa ambavyo vimewezesha wanafunzi wote waliochagulia kuingia madarasani kwa wakati mmoja

Madiwani wakiwasilisha taarifa za kamati

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 05, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI November 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MKATABA January 08, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MKIMBIZA MWENGE KIWILAYA March 30, 2024
  • Soma

Habari mpya

  • DC MNTENJELE AKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO SEKTA YA ELIMU

    June 25, 2025
  • DED MWANZALIMA ATEMBELEA MIRADI YA ELIMU

    June 21, 2025
  • TANDAHIMBA YAPATA HATI SAFI MARA YA TANO MFULULIZO.

    June 17, 2025
  • WAZIRI SIMBACHAWENE AMPONGEZA MKURUGENZI WA TANDAHIMBA NA MADIWANI KWA KUFANYA ZIARA YA MAFUNZO SIMIYU.

    June 11, 2025
  • Soma

Video

MKUU WA WILAYA YA TANDAHIMBA PAMOJA NA MKURUGENZI WASHIRIKI UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAHEHA
Video nyingin

Kurasa za karibu

  • Ijue Tandahimba.

Viungio vinavyousiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • President's Official Website
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya sehemu

Tandahimba District Council

Wasiliana Nasi

    TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA

    Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA

    Simu: +25523 2410030

    Simu:

    Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa