• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
Tandahimba District Council
Tandahimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Idara na Vitengo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Kumuona Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoko kwenye Mpango
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Zabuni
    • Kanuni na Taratifbu
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha habari
    • Habari Mpya
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya picha

Tandahimba waadhimisha siku ya Wanawake katika kijiji cha Likolombe

Posted on: March 9th, 2022

Na Kitengo cha Habari na Mawasailiano

Mkuu wa Wilaya yaTandahimba Mhe Kanali Patrick  Sawala amesema kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa mtu atakayemdhalilisha  na kufanya vitendo vya kikatili kwa wanawake


Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Mhe.Kanali Patrick Sawala akisoma hotuba yake kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake Kiwilaya 

Ameyasema hayo  kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake Kiwilaya ambayo yamefanyika katika kijiji cha Likolombe kata ya Mkwiti ambapo kauli mbiu ya mwaka huu 2022 ni ‘Kizazi cha usawa kwa maendeleo endelevu’

 

Wanawake wakifurahia siku yao kwa kucheza

 “Tutakuwa wakali na tutachukua hatua kali sanakwa mtu ambaye atabainika amedhalilisha na kumfanyia vitendo vya kikatili mwanamke,lakini mjitokeze kugombea nafasi za uongozi kwa nafasi mbalimbali,hii kaulimbiu isibaki kwenye makaratasi  bali itoe matokeo chanya, zingatieni kutimiza wajibu wenu ili muweze kudai haki ”amesema Dc Sawala 

 

Aidha  ameeleza kuwa  pamoja na wingi wa wanawake  kwenye jamii isibaki kwenye namba bali iwe chachu ya kuleta maendeleo na kukataa kuishi kinyonge kwenye dimbwi la umaskini kwa kufanya kazi kwa bidii katika shughuli zinazowaongezea kipato 

 

Dc Sawala akiwa  katika viwanja vya maadhimisho hayo ambapo huduma za uchangiaji damu na utoaji wa elimu na chanjo ya Uviko – 19 ilikuwepo  aliongoza wananchi kuchangia damu na kueleza kuwa  lengo ni kuwasaidia wenye mahitaji hususan mama na mtoto                     

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba Ndugu Mussa Gama  amesema kuwa changamoto ambazo wamezibainisha ikiwemo ujenzi wa bweni la wasichana kwa sekondari ya Mkwiti watalifanyia kazi kwa haraka ili wanafunzi wa kike waweze kukaa shuleni

“Changamoto ya bweni nimeichukua na nimeona umbali uliopo tutalifanyia kazi haraka ili wanafunzi wetu wakae bweni  ili wapate  muda wa kujisomea ni matumaini yangu  kuongeza ufaulu  wa  wanafunzi wetu,”amesema Mkurugenzi

Aidha katika maadhimisho hayo asasi  kama vile Shirika la wanawake wenye uthubutu Tandahimba (WAO),Benki ya wananchi wa Tandahimba (TACOBA) Chama kikuu cha Ushirika tawi la Tandahimba(TANECU)Mbunge waJimbo la Tandahimba Mhe.Katani Katani ,Idara ya maendeleo na Shirika la maendeleo ya michezo mashuleni (SDA)   wamechangia taulo za kike kwa wanafunzi ,fedha kwa ajili ya kumsaidia mtoto mlemavu anayehitaji kiti mwendo, bima za afya za ICHF kwa familia zinazoongozwa na akina mama sambamba na kuwafungulia wanafunzi 10 akaunti ya Tacoba

 






Matangazo

  • TANGAZO LA WALIOFAULU USAILI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. January 15, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI November 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MKATABA January 08, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MKIMBIZA MWENGE KIWILAYA March 30, 2024
  • Soma

Habari mpya

  • DC MNTENJELE AKABIDHI VISHIKWAMBI KWA MAAFISA UGANI TANDAHIMBA

    February 18, 2025
  • KU WILAYA YA TANDAHIMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU MWAKA 2025

    February 17, 2025
  • Vipaumbele Mahususi vya Bajeti ya 2025/2026 Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba.

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI TANDAHIMBA LAPITISHA MAKISIO YA MPANGO NA BAJETI YA TSH .BIL.40.2 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026.

    February 13, 2025
  • Soma

Video

MKUU WA WILAYA YA TANDAHIMBA PAMOJA NA MKURUGENZI WASHIRIKI UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAHEHA
Video nyingin

Kurasa za karibu

  • Ijue Tandahimba.

Viungio vinavyousiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • President's Official Website
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya sehemu

Tandahimba District Council

Wasiliana Nasi

    TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA

    Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA

    Simu: +25523 2410030

    Simu:

    Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa