Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe.Kanali Patrick Sawala leo Juni 10,2025 amekagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari iliyopo Kata ya Mkwedu Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba wenye gharama ya Shilingi Milioni 560.5 ambapo amesistiza kasi iongezeke
Amesema mradi huo ukikamilika kwa wakati wanafunzi wataanza kusoma utapunguza chanamoto wanafunzi kutembea umbali mrefu kufuata shule
Aidha akizungumza na wananchi waliokuwepo kwenye eneo hilo la mradi amewapongeza kwa kushiriki katika utekelezaji wa mradi huo .
Mradi huo unaotekelezwa kupitia Programu ya kuimarisha Elimu ya Sekondari (SEQUIP) unatarajia kuhudumia wanafunzi 320
#Tandahimba tumejipanga kazi zinaendelea
TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA
Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA
Simu: +25523 2410030
Simu:
Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz
Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa