• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
Tandahimba District Council
Tandahimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Idara na Vitengo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Kumuona Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoko kwenye Mpango
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Zabuni
    • Kanuni na Taratifbu
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha habari
    • Habari Mpya
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya picha

Pikipiki 32 zakabidhiwa kwa watendaji kata kuongeza kasi ya ukusanyaji mapato

Posted on: February 10th, 2022

Na Kitengo cha Habari na Mawasiliano

Watendaji kata Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba wametakiwa kuongeza kasi katika ukusanyaji wa  mapato ya ndani  baada ya kukabidhiwa pikipiki 32 zenye thamani ya zaidi ya shilingi Mil.83  fedha ambazo zimetokana na mapato ya ndani

Mwenyekiti  Mhe.Baisa Baisa akimkabidhi pikipiki  katibu wa watendaji ndugu Sudi Sudi

Akikabidhi pikipiki hizo 32 kwa watendaji kata  zote Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba Mhe.Baisa Baisa  ameeleza kuwa fedha zilizotumika kununulia pikipiki hizo zimetokana na mapato ya ndani lakini ziliwekwa kwenye bajeti ya  kununua gari ya Mkurugenzi

Amesema kuwa Mkurugenzi baada ya kuona changamoto iliyopo katika ukusanyaji wa mapato akaridhia fedha hiyo isinunuliwe gari badala yake itumike kuwanunulia vyombo vya usafiri watendaji kata ili ziwasaidie katika ukusanyaji wa mapato

“Nampongeza Mkurugenzi kwa kuridhia na madiwani naamini pikipiki hizi zinakwenda kuleta matokeo mazuri katika ukusanyaji wa mapato ndani ya Wilaya yetu,hatutarajii kusikia tena changamoto ya usafiri kutoka eneo moja kwenda jingine kukusanya mapato,mkazitunze kwakuwa  ni mali ya uma,”amesema Mwenyekiti

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba ndugu Mussa Gama amesema kuwa pikpiki hizo zitawarahisishia watendaji kata kutekeleza majukumu yao ipasavyo hussan ya ukusanyaji mapato ambayo ni lengo kuu

Mkurugenzi Mtendaji ndugu Mussa Gama akiwasha moja ya pikpiki hizo kwa ajili ya majaribio

“Fedha hizi zilitakiwa zinunue gari,lakini nikaona kuwa tuboreshe ukusanyaji wa mapato,watendaji ndiyo wanahusika wa zoezi hilo katika maeneo yao,nikaridhia na nikawashawishi madiwani pia tubadili matumizi haya ili tuongeze mapato ya Halmashauri yetu,lakini pia pikipiki hizi zitawasaidia kufika kwa wakati katika vikao mbalimbali ambavyo wanahitajika Wilayani,kwasababu wengi walikuwa wanachelewa kutokana na changamoto ya usafiri,”amesema Mkurugenzi

Aidha nao watendaji kata ambao leo wamekabidhiwa pikipiki hizo wameushukuru Uongozi wa Halmashauri  lakini pia wamesema  usafiri kutoka eneo moja kwenda lingine ilikuwa ni changamoto katika kutekeleza majukumu yao

Matangazo

  • TANGAZO LA WALIOFAULU USAILI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. January 15, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI November 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MKATABA January 08, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MKIMBIZA MWENGE KIWILAYA March 30, 2024
  • Soma

Habari mpya

  • DC MNTENJELE AKABIDHI VISHIKWAMBI KWA MAAFISA UGANI TANDAHIMBA

    February 18, 2025
  • KU WILAYA YA TANDAHIMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU MWAKA 2025

    February 17, 2025
  • Vipaumbele Mahususi vya Bajeti ya 2025/2026 Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba.

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI TANDAHIMBA LAPITISHA MAKISIO YA MPANGO NA BAJETI YA TSH .BIL.40.2 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026.

    February 13, 2025
  • Soma

Video

MKUU WA WILAYA YA TANDAHIMBA PAMOJA NA MKURUGENZI WASHIRIKI UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAHEHA
Video nyingin

Kurasa za karibu

  • Ijue Tandahimba.

Viungio vinavyousiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • President's Official Website
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya sehemu

Tandahimba District Council

Wasiliana Nasi

    TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA

    Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA

    Simu: +25523 2410030

    Simu:

    Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa