• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
Tandahimba District Council
Tandahimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Idara na Vitengo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Kumuona Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoko kwenye Mpango
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Zabuni
    • Kanuni na Taratifbu
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha habari
    • Habari Mpya
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya picha

NMB TAWI LA TANDAHIMBA YAKABIDHI MADAWATI ,STULI NA MABATI KWA SEKTA YA ELIMU

Posted on: November 7th, 2023

Na Kitengo cha Mawasiliano 

Mkuu wa Wilaya ya  Tandahimba Mhe.Kanali Patrick Sawala amepokea mabati  369,madawaati 390 na stuli za maabara 100 zote zikiwa na thamani ya Tsh Milioni 63.9 kutoka  Benki ya NMB tawi la Tandahimba ikiwa ni mchango wao kwa sekta ya elimu kuunga juhudi za Serikali katika sekta hiyo.

Akizungumza Novemba 7,2023  kwenye Hafla fupi ya makabidhiano ya vifaa hivyo yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri na kuhudhuriwa na Wakuu wa Idara na watumishi Dc Sawala ameipongeza  benki ya NMB kwa  vifaa hivyo ambapo amesema vitasaidia katika ujifunzaji na ufundishaji katika shule hizo.

" Nawapongeza sana Benki ya Nmb kwa mchango huu wa madawati,mabati na stuli za maabara ambazo zinakwenda kupunguza uhaba kwenye  shule  zetu,wito kwa taasisi nyingine kuiga mfano wa NMB wa kurudisha kwa jamii,ili kuendelea kuunga juhudi za Serikali katika Sekta ya Elimu" amesema Dc Sawala.

Kwa upande wake Meneja wa Benki ya NMB  Kanda ya Kusini Ndg.Faraja Ng'ingo akikabidhi vifaa hivyo amesema kuwa benki hiyo imekuwa na utaratibu wa kurudisha faida ya asilimia 1 wanayoipata kwa jamii ambapo wanachangia katika sekta ya Elimu na Afya kama sehemu ya uwajibikaji kwa jamii inayowazunguka.

" Tunatambua juhudi  za Serikali ya awamu ya sita ya kusimamia upatikanaji wa Elimu bora kwa nguvu zote,hatuna budi kuipongeza Serikali kwa hilo na sisi kama wadau tunao wajibu wa kuunga mkono juhudi hizi za Maendeleo kwani jamii imeifanya Benki ya NMB kuwa hapa tulipo," amesema Meneja wa Kanda


Matangazo

  • TANGAZO LA WALIOFAULU USAILI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. January 15, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI November 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MKATABA January 08, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MKIMBIZA MWENGE KIWILAYA March 30, 2024
  • Soma

Habari mpya

  • DC MNTENJELE AKABIDHI VISHIKWAMBI KWA MAAFISA UGANI TANDAHIMBA

    February 18, 2025
  • KU WILAYA YA TANDAHIMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU MWAKA 2025

    February 17, 2025
  • Vipaumbele Mahususi vya Bajeti ya 2025/2026 Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba.

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI TANDAHIMBA LAPITISHA MAKISIO YA MPANGO NA BAJETI YA TSH .BIL.40.2 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026.

    February 13, 2025
  • Soma

Video

MKUU WA WILAYA YA TANDAHIMBA PAMOJA NA MKURUGENZI WASHIRIKI UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAHEHA
Video nyingin

Kurasa za karibu

  • Ijue Tandahimba.

Viungio vinavyousiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • President's Official Website
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya sehemu

Tandahimba District Council

Wasiliana Nasi

    TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA

    Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA

    Simu: +25523 2410030

    Simu:

    Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa