Mei 22, 2025
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Ismail Ali Ussi ameridhia kuweka jiwe la msingi kwenye Mradi wa Maji Mivanga Halmashauri ya Tandahimba wenye thamani ya Tsh. Milioni 455 fedha kutoka Serikali Kuu kupitia programu ya lipa kwa matokeo(P4R) sambamba na wadau mbalimbali wa Maji ambao unatarajia kuwanufaisha wananchi wapatao 2750 wa kijiji cha Mivanga.
Akizungumza na wananchi wa Mivanga kiongozi wa mbio za Mwenge wa uhuru kitaifa amesema dhamira ya Rais Samia ni njema katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji safi na salama mijini na vijijini na ndio maana anatoa fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya maji.
Aidha, Amewasisitiza wananchi kuhakikisha wanaitunza miundombinu ya maji ili iweze kudumu kwa muda mrefu .
"Unapomuona mtu anaharibu miundombinu toa taarifa kwa mamlaka husika ili aweze kuchukuliwa hatua za kisheria, nawaomba sana tuitunze na kuilinda miundombinu hii" Ussi
Kwa upande wake Mbunge wa jimbo la Tandahimba Mhe.Katani Katani ameishukuru serikali ya awamu ya Sita chini ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha za ujenzi wa miradi mingi ya maji ukiwemo wa Mivanga .
Kaulimbiu: Jitokeze kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 kwa Amani na Utulivu
TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA
Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA
Simu: +25523 2410030
Simu:
Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz
Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa