• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
Tandahimba District Council
Tandahimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Idara na Vitengo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Kumuona Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoko kwenye Mpango
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Zabuni
    • Kanuni na Taratifbu
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha habari
    • Habari Mpya
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya picha

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara akabidhi Pikipiki 64 kwa maafisa Ugani Tandahimba

Posted on: March 10th, 2023

Na Kitengo cha Mawasiliano

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe.Kanali Ahmed Abbas Ahmed amewataka maafisa ugani waliokabidhiwa pikipiki kuzitumia kama ilivyokusudiwa ili kutoa elimu na ushauri wa kitaalamu kwa wakulima waweze kuongeza uzalishaji sambamba na  kuzingatia sheria ,taratibu na kanuni za matumizi ya vifaa vya Serikali

Amezungumza  hayo Machi 10,2023 wakati akikabidhi pikpiki 34 kwa maafisa ugani katika kijiji cha Nanhyanga Kata ya Nanhyanga  Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba ambapo Pikipiki hizo zimetolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt Samia Suluhu Hassan kupitia Wizara ya Kilimo

Mhe.Kanali Ahmed amesema kwamba  pikipiki zinawezesha maafisa ugani  kuwafikia wakulima katika mashamba yao ili kutoa ushauri wa kitaalamu katika kuongeza mnyororo wa thamani na ufanisi wa kilimo kwa wakati ili  kuongeza uzalishaji wa mazao

Aidha Mkuu wa Mkoa akiwa  Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba katika ziara yake ya siku moja ametembelea  mashamba  mawili ya mfano ya zao la Korosho na kuzungumza na wananchi wa Nanhyanga  ambapo amewasistiza kuendelea na operesheni ya “Ondoa mapori ongeza Uzalishaji” kwa kuzingatia matumizi ya mbegu bora na upandaji wa kufuata ushauri wa wataalamu wa kilimo

RC akijibu kero za wananchi ambazo ziliwasilishwa na Mbunge wa Jimbo la Tandahimba Mhe.Katani Katani na Diwani wa Kata hiyo Mhe.Abbas Namaneha  katika kikao hicho amewataka waendesha pikipiki (bodaboda) kuzingatia sheria za barabarani lakini pia Jeshi la Polisi kitengo cha Usalama wa barabarani kusimamia sharia,haki na busara katika kutekeleza majukumu yao

Matangazo

  • TANGAZO LA WALIOFAULU USAILI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. January 15, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI November 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MKATABA January 08, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MKIMBIZA MWENGE KIWILAYA March 30, 2024
  • Soma

Habari mpya

  • MWENGE WARIDHIA KUWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI MIVANGA UTAKAONUFAISHA ZAIDI YA WANANCHI 2000.

    May 22, 2025
  • USAFI MWISHO WAWEZI

    May 31, 2025
  • DC MNTENJELE AKABIDHI VISHIKWAMBI KWA MAAFISA UGANI TANDAHIMBA

    February 18, 2025
  • KU WILAYA YA TANDAHIMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU MWAKA 2025

    February 17, 2025
  • Soma

Video

MKUU WA WILAYA YA TANDAHIMBA PAMOJA NA MKURUGENZI WASHIRIKI UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAHEHA
Video nyingin

Kurasa za karibu

  • Ijue Tandahimba.

Viungio vinavyousiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • President's Official Website
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya sehemu

Tandahimba District Council

Wasiliana Nasi

    TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA

    Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA

    Simu: +25523 2410030

    Simu:

    Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa