• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
Tandahimba District Council
Tandahimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Idara na Vitengo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Kumuona Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoko kwenye Mpango
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Zabuni
    • Kanuni na Taratifbu
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha habari
    • Habari Mpya
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya picha

Madiwani Tandahimba waicharukia Tarura

Posted on: April 23rd, 2020


Na. Kitengo cha Habari na mawasiliano 

Baraza la madiwani  Halmashauri ya Tandahimba   wameiomba  serikali kupitia Wakala wa barabara vijijini na mijini (Tarura) kufanya maboresho ya barabara  kwa kuzichonga hususani maeneo ya vijijini  ambayo kwa sasa  hayafikiki kutokana na ubovu wa miundombinu hiyo


Akielezea changamoto ya barabara Diwani  wa kata ya Mihuta  Hamisi Mfaume amesema kuwa miaka  iliyopita  barabara hizo zilikuwa zinapitika ndani ya vijiji lakini kwa sasa barabara nyingi za ndani ya Wilaya zimejifunga na kuwapa tabu wananchi kutoka sehemu moja kwenda nyingine

“Tunawaomba Tarura walichukulie suala  la barabara  vijijini kama dharura hususan wakati huu wa ugonjwa wa corona (Covid – 19)  barabara zimejifunga tunapata tabu kupata huduma mbalimbali  ,”amesema Mfaume


Amesema awali Halmashauri ilikuwa inajitahidi kuzichonga barabara hizo  na kuwawezesha wananchi kuendelea na shughuli zao za maendeleo  lakini kwa sasa barabara hizo  zimeharibika hata upitaji  wa gari na pikipiki ni mgumu

“Wakati barabara hizi zipo chini ya Halmashauri zilikuwa zinapitika na zikiharibika walikuwa wajitahidi kuzichonga lakini kwa sasa Tandahimba ipo  kwenye kisiwa kutokana na ubovu wa barabara ”,amesema Mfaume

 

Naye Mhandisi wa Tarura Wilaya Paulo Mliya akijibu hoja za madiwani amesema wanayajua maeneo yote mabovu hivyo watayashughulia mara baada ya kupata  fedha 

“Tunayajua  maeneo ambayo hayapikiti kama vile Kata ya Mdimba na Chingungwe tutayashughulikia  kwa sasa mtuvumilie,”amesema Mliya

 



 

Baraza la madiwani limefanyika jana  katika ukumbi wa Halmashauri ya Tandahimba  na wameweza kupitisha agenda mbalimbali sambamba na kupeana  msistizo wa kuendelea kuwaelimisha wananchi katika maeneo waliyopo kuhusu ugonjwa wa Corona (Covid – 19)

 

Matangazo

  • TANGAZO LA WALIOFAULU USAILI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. January 15, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI November 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MKATABA January 08, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MKIMBIZA MWENGE KIWILAYA March 30, 2024
  • Soma

Habari mpya

  • DC MNTENJELE AKABIDHI VISHIKWAMBI KWA MAAFISA UGANI TANDAHIMBA

    February 18, 2025
  • KU WILAYA YA TANDAHIMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU MWAKA 2025

    February 17, 2025
  • Vipaumbele Mahususi vya Bajeti ya 2025/2026 Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba.

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI TANDAHIMBA LAPITISHA MAKISIO YA MPANGO NA BAJETI YA TSH .BIL.40.2 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026.

    February 13, 2025
  • Soma

Video

MKUU WA WILAYA YA TANDAHIMBA PAMOJA NA MKURUGENZI WASHIRIKI UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAHEHA
Video nyingin

Kurasa za karibu

  • Ijue Tandahimba.

Viungio vinavyousiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • President's Official Website
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya sehemu

Tandahimba District Council

Wasiliana Nasi

    TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA

    Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA

    Simu: +25523 2410030

    Simu:

    Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa