• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
Tandahimba District Council
Tandahimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Idara na Vitengo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Kumuona Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoko kwenye Mpango
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Zabuni
    • Kanuni na Taratifbu
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha habari
    • Habari Mpya
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya picha

MAAFISA UGANI KILIMO WALIOAJIRIWA NA BODI YA KOROSHO (CBT) WAPEWA MAFUNZO TANDAHIMBA.

Posted on: January 13th, 2025

Maafisa Ugani kilimo 51 walioajiriwa na Bodi ya Korosho Tanzania (CBT)  wamepewa mafunzo ya kuwajengea uwezo ili kwenda kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi katika Kata walizopangiwa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba .

Akisoma taarifa ya  ufunguzi wa mafunzo hayo leo Januari 13,2025 Mwakilishi wa Mkuu wa  Wilaya ya Tandahimba Ndg.Francis Mkuti amewataka maafisa ugani hao ambao watakwenda kwenye Kata zote za Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba kuzingatia mafunzo hayo ili kwenda kuongeza uzalishaji wa zao la korosho .

" Napenda kuwapongeza Bodi ya Korosho  Tanzania kwa usimamizi mzuri wa korosho kwa ongezeko la uzalishaji ambapo msimu huu wa mwaka  2024/2025  tumeshuhudia ongezeko kutoka Tani 310,787  mwaka 2023/2024  hadi kufikia Tani 410,000  mwaka 2024/2025 hivyo maafisa ugani hawa watakuwa chachu ya kuongeza uzalishaji lakini pia mkatumie nafasi mliyopata kuonesha uzalendo wenu kwa wakulima wetu kwa kufanya kazi kwa  juhudi kubwa pia mtaongeza ujuI na kupata uzoefu  wa  ufikishaji wa huduma za ugani kwa wakulima ili wazalishe kwa tija mazaonwanayolima likiwemo Korosho,"

Kwa upande wake Afisa Kilimo wa bodi ya korosho Ndg.Johnson Kaaya amesema  mafunzo rejea ya maafisa ugani  hao ni mpango wa kukuza ujuzi kwenye Programu ya Jenga kesho iliyo bora ambapo baada ya kuwajengea uwezo waende wakatekeleze kwa vitendo ili kuongeza uzalishaji wa zao la korosho.

Aidha amesema  mpango wa kuajiri maafisa ugani hao ni kuongeza uzalishaji wa korosho ghafi nchini kufikia Tani 700,000 mwaka 2025/2026 na Tani 1,000,000 ifikapo mwaka 2029/2030. " Maafisa ugani hawa  katika kuhakikisha wanaleta mabadiliko chanya watakabidhiwa vitendea kazi  ambavyo ni pikipiki na vishikwambi ili wakatekeleze shughuli za uendeshaji wa zao la Korosho," amesema Kaaya

Mafunzo hayo ya siku tano  kwa Maafisa Ugani  yatahitimishwa  Januari 17,2025

#Tandahimba tumejipanga kazi zinaendelea

Matangazo

  • TANGAZO LA WALIOFAULU USAILI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. January 15, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI November 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MKATABA January 08, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MKIMBIZA MWENGE KIWILAYA March 30, 2024
  • Soma

Habari mpya

  • DC MNTENJELE AKABIDHI VISHIKWAMBI KWA MAAFISA UGANI TANDAHIMBA

    February 18, 2025
  • KU WILAYA YA TANDAHIMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU MWAKA 2025

    February 17, 2025
  • Vipaumbele Mahususi vya Bajeti ya 2025/2026 Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba.

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI TANDAHIMBA LAPITISHA MAKISIO YA MPANGO NA BAJETI YA TSH .BIL.40.2 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026.

    February 13, 2025
  • Soma

Video

MKUU WA WILAYA YA TANDAHIMBA PAMOJA NA MKURUGENZI WASHIRIKI UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAHEHA
Video nyingin

Kurasa za karibu

  • Ijue Tandahimba.

Viungio vinavyousiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • President's Official Website
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya sehemu

Tandahimba District Council

Wasiliana Nasi

    TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA

    Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA

    Simu: +25523 2410030

    Simu:

    Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa