• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
Tandahimba District Council
Tandahimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Idara na Vitengo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Kumuona Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoko kwenye Mpango
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Zabuni
    • Kanuni na Taratifbu
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha habari
    • Habari Mpya
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya picha

Kiasi cha Tsh.Mil 70 za Mfuko wa Elimu Halmashauri ya Tandahimba zatengeneza madawati 1000

Posted on: November 2nd, 2022

Na Kitengo cha Mawasiliano

Kiasi cha Shilingi Milioni 70 za Mfuko wa Elimu wa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba zimetumika kutengeneza madawati  1000  ya wanafunzi wa Shule za Msingi

Akikabidhi madawati 300 ya awamu ya kwanza kwa shule kumi za Msingi  Nov 2,2022 Mhe.Mohamed Namgugu Diwani wa Kata ya Mahuta  ambapo amekabidhi kwa niaba ya Mwenyekiti wa Halmashauri amesema kuwa madawati yao ni moja ya faida za uchangiaji wa mfuko wa Elimu wa Halmsahauri

“Mfuko huu wachangiaji wakubwa ni Wakulima wa Tandahimba  kwaiyo leo tunakabidhi madawati haya 300 kwa shule za Msingi ili wanafunzi wetu wakae  huku mengine yakimaliziwa,Mfuko huu unatusaidia wanatandahimba tuendelee kuchanhia mfuko huu ili uzidi kufanya vitu vikubwa katika kuboresha Elimu ndani ya Wil,aya yetu,”amesema Mhe.Namgugu

Naye Mkuu wa Idara ya Elimu Awali  na Msingi  Ndg Samwel Mshana akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmasahauri ametoa wito kwa Walimu Wakuu kuyatunza madawati hayo ili yaweze kuwasaidia wanafunzi

Aidha Naye Mwl.Shamsia Mohamed akizungumza kwa niaba ya Walimu Wakuu wengine ambao wamekabidhiwa madawati hayo wameshukuru na kuupongeza hatua hiyo ambapo amebaisha  kuwa madawati hayo yatapunguza changamoto ya madawati katika shule zao

Hata hivyo  Ndg.Dadi Dadi Mkazi wa Mahuta amepongeza hatua hiyo na kutoa rai kwa wakulima na wanachi wa Tandahimba kuendelea kuchangia mfuko wa Elimu ili uweze kuleta maboresho katika Elimu ndani ya Wilaya ya Tandahimba

Shule za Msingi ambazo zimepokea  madawati hayo ni Nanhyanga A,Nanhyanga B,Namkomolela,Mndumbwe,Mahuta Bondeni,Majengo,Mkonjowano,Nachunyu,Malamba na Mkulung’ulu

Matangazo

  • TANGAZO LA WALIOFAULU USAILI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. January 15, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI November 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MKATABA January 08, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MKIMBIZA MWENGE KIWILAYA March 30, 2024
  • Soma

Habari mpya

  • DC MNTENJELE AKABIDHI VISHIKWAMBI KWA MAAFISA UGANI TANDAHIMBA

    February 18, 2025
  • KU WILAYA YA TANDAHIMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU MWAKA 2025

    February 17, 2025
  • Vipaumbele Mahususi vya Bajeti ya 2025/2026 Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba.

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI TANDAHIMBA LAPITISHA MAKISIO YA MPANGO NA BAJETI YA TSH .BIL.40.2 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026.

    February 13, 2025
  • Soma

Video

MKUU WA WILAYA YA TANDAHIMBA PAMOJA NA MKURUGENZI WASHIRIKI UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAHEHA
Video nyingin

Kurasa za karibu

  • Ijue Tandahimba.

Viungio vinavyousiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • President's Official Website
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya sehemu

Tandahimba District Council

Wasiliana Nasi

    TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA

    Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA

    Simu: +25523 2410030

    Simu:

    Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa