Na Kitengo cha Mawasiliano
Wauguzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba wameungana na Wauguzi duniani kusherekea siku ya Wauguzi kwa kufanya shughuli za kijamii pamoja na kutoa zawadi mbalimbali kwa wagonjwa wa Hospitali ya Wilaya ya Tandahimba
Akizungumza kwenye maadhimisho hayo ya Kiwilaya ambayo yamefanyika katika Hospitali ya Wilaya Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Mei 12,2023 Mhe.Patrick Sawala ametoa wito kwa wauguzi kuendelea kutoa huduma kwa kuzingatia maadili ya kazi zao na upendo kwa wagonjwa
“Nawapongezeni wauguzi kwa kazi nzuri mnazofanya ombi langu endeleeni kuifanya hiyo kazi ya kuwahudumia wananchi kwa huruma na upendo,lakini nitumie fursa hii kumshukuru Mhe.Rais kwa ukuzaji na uboreshaji wa sekta ya afya katika Wilaya yetu”amesema Dc Sawala
Aidha naye Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba Ndg.Mussa Gama amewapongeza kwa kuadhimisha siku yao ya wauguzi na kuwaahidi ushauri waliotoa katika taarifa yao utashughulikiwa
Wauguzi wameadhimisha kwa maandamano kuanzia ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba na kupokelewa na Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Mhe.Kanali Patrick Sawala katika hospitali ya Wilaya ambapo Kauli mbiu ya mwaka 2023 "WAUGUZI WETU MUSTAKABALI WETU"
TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA
Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA
Simu: +25523 2410030
Simu:
Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz
Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa