• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
Tandahimba District Council
Tandahimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Idara na Vitengo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Kumuona Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoko kwenye Mpango
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Zabuni
    • Kanuni na Taratifbu
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha habari
    • Habari Mpya
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya picha

Halmashauri ya Tandahimba yaweka mikakati kuongeza uzalishaji zao la korosho

Posted on: April 24th, 2021

Na Kitengo cha Habari na Mawasiliano 

Mikorosho 53,360  katika Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba imekatwa  kuboresha uzalishaji wa zao la korosho ambapo idadi ya miche 33,893 imebebeshwa na miche 30,223 imepandwa  ikiwa ni mkakati wa kuongeza uzalishaji wa zao hilo.

Baraza la madiwani wa Halmasahauri ya Tandahimba wakiwa kwenye kikao cha kawaida cha baraza ya robo ya tatu

Akiwasilisha taarifa hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji,Afisa Mipango Wilaya Hassan Nzyungu kwenye kikao cha kawaida cha baraza la madiwani  kilichofanyika ukumbi wa mikutano  ameeleza kuwa  ukubwa wa hekta 29.5 imefufuliwa na mashamba yenye ukubwa hekta 655 yameanzishwa

Afisa Mipango Hassan Nzyungu (aliyesimama) akieleza jambo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji

Kaimu Afisa Kilimo na Ushirika Haroun Kisimba akijibu swali la Diwani wa Chikongola Yahaya Mussa  la kushuka kwa zao la korosho kwa miaka mitatu mfululuzo amesema kuwa sababu mojawapo ni mabadiliko ya tabia ya nchi, mvua kunyesha chini ya milimita 900 imechangia kushuka kwa uzalishaji,mvua za vuli za mwezi wa 9-10 zilisababisha kuangusha maua na korosho changa na  uwepo wa mikorosho mizee  lakini tayari Halmashauri imechukua hatua kuboresha zao hilo

Wakuu wa Idara na vitengo wakisikiliza kikao cha baraza la madiwani  katika ukumbi wa Halmasahauri

Aidha naye Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Sebastian Waryuba amewapongeza madiwani kwa kuendelea kusimamia wananchi katika masuala ya maendeleo na shughuli za kilimo  katika kata zao na kusistiza kuwa wataalam wahakikishe pembejeo zinawafikia wakulima kwa wakati 

Mkuu wa Wilaya Mhe.Sebastian Waryuba akieleza jambo kwenye baraza la madiwani

Mwenyekiti wa Halmasahauri ya Tandahimba Baisa Baisa amesistiza  ushirikiano  uendelee kuimarika kwa Wakuu wa Idara ,madiwani na watumishi ili kuwaletea wananchi wa Tandahimba maendeleo

Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe.Baisa Baisa akizungumza kwenye baraza hilo

Halmashauri ya Tandahimba  kwa upande wa korosho msimu 2018/2019 ilizalishatani 37,650 za korosho ghafi ukilinganisha na tani 37,367 msimu 2019/2020  kwa msimu mwaka 2020/2021 kwa minada 15 ambayo ilifanyika tani 29,433.5  zenye thamani ya  Tsh 68,875,132,501.40

Matangazo

  • TANGAZO LA WALIOFAULU USAILI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. January 15, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI November 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MKATABA January 08, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MKIMBIZA MWENGE KIWILAYA March 30, 2024
  • Soma

Habari mpya

  • DC MNTENJELE AKABIDHI VISHIKWAMBI KWA MAAFISA UGANI TANDAHIMBA

    February 18, 2025
  • KU WILAYA YA TANDAHIMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU MWAKA 2025

    February 17, 2025
  • Vipaumbele Mahususi vya Bajeti ya 2025/2026 Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba.

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI TANDAHIMBA LAPITISHA MAKISIO YA MPANGO NA BAJETI YA TSH .BIL.40.2 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026.

    February 13, 2025
  • Soma

Video

MKUU WA WILAYA YA TANDAHIMBA PAMOJA NA MKURUGENZI WASHIRIKI UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAHEHA
Video nyingin

Kurasa za karibu

  • Ijue Tandahimba.

Viungio vinavyousiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • President's Official Website
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya sehemu

Tandahimba District Council

Wasiliana Nasi

    TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA

    Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA

    Simu: +25523 2410030

    Simu:

    Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa