• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
Tandahimba District Council
Tandahimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Idara na Vitengo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Kumuona Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoko kwenye Mpango
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Zabuni
    • Kanuni na Taratifbu
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha habari
    • Habari Mpya
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya picha

Halmashauri ya Tandahimba yatoa msaada wa matibabu kwa kijana aliyepata ajali ya gari

Posted on: April 15th, 2020

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Tandahimba Said Msomoka


Na Kitengo cha Habari na Mawasiliano

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Tandahimba  Said Msomoka ametoa msaada wa matibabu kwa kijana Said Abdallah  ambaye alipata ajali iliyosababisha kuvunjika kwa miguu miwili na mkono  lakini kwa muda wa miezi miwili hakupata huduma stahiki kwa kukosa fedha za matibabu

Akizungumza ofisini kwake  Msomoka amesema kuwa amechukua hatua hiyo baada ya Mwenyekiti wa  Kitongoji chaTandahimba mjini Ashura Madata kutoa taarifa za uwepo wa kijana huyo katika kitongoji chake

Kijana Said Nyecha (29) ambaye aligongwa na gari miezi miwili iliyopita

Amesema kuwa  Halmashauri imeamua kumuhudumia  kijana huyo  ili aweze kupata matibabu stahiki kwakuwa kidonda hicho hakijapata huduma kwa muda  hivyo ameamua  kuchukua hatua ya kumpeleka Hospitali ya Wilaya kwa hatua za awali  na baadaye atampelekwa  Hospitali ya Nyangao

“Tumechukua hatua ya kumkatia bima ya ICHF ili aweze kupata huduma nafuu kwakuwa   mzazi  wakeambaye ni (mama) kutokuwa na uwezo wa kumudu gharama zake,kwaiyo walipewa matibabu nusu kule Hospitali ya Nyangao sisi tutamalizia fedha yote inayodaiwa hospitali na tutawapa fedha zingine za kuendelea na matibabu sambamba na  chakula chake kwa kipindi atakachokuwa hospital,”amesema Msomoka

Naye mama yake Halima Ally amesema kijana wake amegongwa na gari kuanzia mwezi wa pili mwaka huu  na gari lilikimbia kwaiyo alipelekwa hospitali kutokana na kukosa fedha hakuweza kupata matibabu mazuri na hivyo kurudi nyumbani 

Mratibu wa mfuko wa  afya ulioboreshwa (ICHF) Violeth Mahembe akiwakabidhi bima ambayo atapata matibabu bure mgonjwa na mama yake ambayo imelipiwa na Halmashauri

“Naishukuru Halmashauri kwa kumpatia Bima itakayomuwezesha kupata huduma , Mkurugenzi  ameridhia kutulipia deni katika Hospitali ya Nyangao ambayo tunadaiwa,kijana wangu amekuwa akiteseka  kwa maumivu makali kwakutopata huduma kwa miezi yote miwili,tunaishukuru serikali kwa msaada huu,”amesema Ally.

Hata hivyo mwenyekiti wa kitongoji Ashura Madata ameeleza kuwa hatua hiyo inaonyesha  serikali ipo karibu na wananchi wake  kwa kuwasaidia pale ambapo wameshindwa kwa kutambua nguvu ya nchi ni vijana

Afisa ustawi wa jamii Gift Limbanga (kushoto)akimkabidhi kwa niaba ya Mkurugenzi fedha taslimu shilingi laki tano kwa ajili ya kuanzia matibabu (kulia) mwenyekiti wa kitongoji cha Tandahimba Ashura Madata

“Huyu kijana ameteseka,vidonda havikuwa vinasafishwa,mkono umevunjika hajafanyiwa chochote na miguu yote miwili  imevunjika kwakuwa uwezo wa mama  yake ni mdogo  alikuwa anakaa naye nyumbani tu,lakini leo tumepata msaada huu tunaishukuru sana halmashauri yetu kwakuwa Mkurugenzi ametoa gari ili aweze kwenda hospitali ya Wilaya kwa ajili ya kusafisha na baadaye atapelekwa hospital ya Nyangao,”amesema Madata

Matangazo

  • TANGAZO LA WALIOFAULU USAILI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. January 15, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI November 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MKATABA January 08, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MKIMBIZA MWENGE KIWILAYA March 30, 2024
  • Soma

Habari mpya

  • DC MNTENJELE AKABIDHI VISHIKWAMBI KWA MAAFISA UGANI TANDAHIMBA

    February 18, 2025
  • KU WILAYA YA TANDAHIMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU MWAKA 2025

    February 17, 2025
  • Vipaumbele Mahususi vya Bajeti ya 2025/2026 Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba.

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI TANDAHIMBA LAPITISHA MAKISIO YA MPANGO NA BAJETI YA TSH .BIL.40.2 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026.

    February 13, 2025
  • Soma

Video

MKUU WA WILAYA YA TANDAHIMBA PAMOJA NA MKURUGENZI WASHIRIKI UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAHEHA
Video nyingin

Kurasa za karibu

  • Ijue Tandahimba.

Viungio vinavyousiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • President's Official Website
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya sehemu

Tandahimba District Council

Wasiliana Nasi

    TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA

    Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA

    Simu: +25523 2410030

    Simu:

    Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa