• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
Tandahimba District Council
Tandahimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Idara na Vitengo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Kumuona Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoko kwenye Mpango
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Zabuni
    • Kanuni na Taratifbu
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha habari
    • Habari Mpya
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya picha

Halmashauri ya Tandahimba yakabidhi viti 800 kwa Walimu na magodoro 48 kwa walimu wapya

Posted on: January 30th, 2021

Na Kitengo cha Habari na Mawasiliano

Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba imetumia kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 55  kuwalipa  fedha  ya kujikimu   walimu wapya 48 , ununuzi wa magodoro kwa ajili ya walimu hao  sambamba na ununuzi wa viti  800 vya walimu wa shule za sekondari na msingi

Viti 800 ambavyo vimenunuliwa kwa ajili ya kukalia walimu wa shule ya msingi na sekondari

Katika Hafla Hiyo Halmashauri  imekabidhi vifaa vya kufundishia na kuchezea watoto wenye mahitaji maalum  shule ya msingi Mjimpya Maalum na Mahuta vifaa ambavyo vimetolewa na Ofisi ya Tamisemi pia  Halmashauri imetoa kiasi cha shilingi Milioni 20 kwa ajili ya ujenzi wa jiko na bwalo

 

Mkuu wa Wilaya Sebastian Waryuba akiwa tayari kukabidhi magodoro hayo kwa walimu

Akikabidhi vifaa hivyo Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Sebastian Waryuba amesema kuwa anaipongeza Halmashauri kwa jitihhada wanazozifanya  kuboresha mazingira kwa Walimu wapya na walimu waliopo

Dc Sebastian  Waryuba akimkabidhi mwalimu wa ajira mpya godoro

“Naipongeza Halmashauri kwa  hatua hii ya kuwapa motisha walimu wapya magodoro kwa ajili ya kuanza maisha ,hii inawatia moyo wa kufanya kazi  lakini hamkuwasahau walimuwaliopo kwakweli tulifanya ziara shule nyingi hawakuwa na viti vya walimu lakini naamini viti hivi vitawasaidia walimu wetu ,”amesema Dc Waryuba

Dc Warryuba (aliyesimama) akimpongeza Mkurugenzi Mtendaji ndugu Said Msomoka

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Tandahaimba ndugu Said Msomoka amesema kuwa fedha hizo zimetoka kwenye mfuko wa Elimu  na  kila mwalimu amepata godoro moja miongoni mwa 48 ambao 22 ni shule msingi na 26 ni sekondari

Mkurugenzi Mtendaji ndugu Said Msomoka akiwasistiza waendelee kutekeleza wajibu wao kwa wananfunzi

“Tumefanya haya ili  kuwarahisishia walimu hawa wapatae mahali pa kujihifadhi lakini pia viti vitawasaidia walimu  katika ofisi zao tulitembelea katika shule mbalimbali tukabaini kuna uhaba wa viti  vya walimu kwaiyo tumenunua  ili waweze kukaa katika mazingira bora,”amesema Ndg Msomoka

Dc Waryuba akiwa pamoja na Mkurugenzi Mtendaji ndg Msomoka wakimkabidhi kiti mwalimu

Aidha amesema viti 800 vina thamani ya shilingi  27,999,984,magodoro 48 kwa walimu ajira mpya   thamani yake  shilingi 7,440,000,kiasi cha shilingi 22,892,000 kwa ajili ya posho ya kujikimu kwa walimu wa ajira mpya na kiasi cha shilingi 20,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa bwalo la wanafunzi wenye mahitaji maalum fedha hizo zimetolewa kwenye mfuko wa elimu

Dc Waryuba akiwakabidhi vifaa vya kufundishia walimu wakuu wa shule ya mahitaji maalum Mjimpya na Mahuta

Hata hivyo walimu wa ajira mpya wameishukuru Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba kwa kuwajali kwa kuwalipa fedha za kujikimu kwa wakati na  magodoro hasa katika kipindi ambacho ni wageni katika maeneo ambayo wameripoti

Matangazo

  • TANGAZO LA WALIOFAULU USAILI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. January 15, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI November 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MKATABA January 08, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MKIMBIZA MWENGE KIWILAYA March 30, 2024
  • Soma

Habari mpya

  • DC MNTENJELE AKABIDHI VISHIKWAMBI KWA MAAFISA UGANI TANDAHIMBA

    February 18, 2025
  • KU WILAYA YA TANDAHIMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU MWAKA 2025

    February 17, 2025
  • Vipaumbele Mahususi vya Bajeti ya 2025/2026 Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba.

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI TANDAHIMBA LAPITISHA MAKISIO YA MPANGO NA BAJETI YA TSH .BIL.40.2 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026.

    February 13, 2025
  • Soma

Video

MKUU WA WILAYA YA TANDAHIMBA PAMOJA NA MKURUGENZI WASHIRIKI UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAHEHA
Video nyingin

Kurasa za karibu

  • Ijue Tandahimba.

Viungio vinavyousiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • President's Official Website
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya sehemu

Tandahimba District Council

Wasiliana Nasi

    TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA

    Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA

    Simu: +25523 2410030

    Simu:

    Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa