• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
Tandahimba District Council
Tandahimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Idara na Vitengo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Kumuona Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoko kwenye Mpango
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Zabuni
    • Kanuni na Taratifbu
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha habari
    • Habari Mpya
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya picha

Dc Waryuba :Boresheni Mila zenu kuepuka mimba za utotoni

Posted on: July 17th, 2020

Na Kitengo cha Habari na Mawasiliano

Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Sebastian Waryuba amesema ataendelea kuwakamata wazazi pande zote mbili mara binti wa shule akipatikana na ujauzito ili kukomesha vitendo vya mimba za utotoni na amewataka kuboresha mila zao kwa kuacha kuwafundisha watoto  mila potofu

Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Sebastian Waryuba akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mambamba na Majengo

Ameyasema hayo wakati akijibu kero ya Hamis Linangwa mkazi wa Ching`ati Kata ya Namikupa aliyehoji  kwanini mzazi akamatwe mara mtoto anapopata ujauzito wakati  mzazi hausiki

Dc Waryuba amesema mila hiyo ya kuwafundisha watoto wa kike vitu ambavyo vipo juu ya uwezo wao ndiyo inayosababisha watoto  kupata ujauzito wakiwa bado shule na kuolewa wakiwa na umri mdogo

Dc Waryuba akizungumza na wananchi wa kijiji cha Chihangi na Namikupa

“Kuna baadhi ya vipengele  katika Mila zenu zinahitaji maboresho,boresheni hii mila ya chikuvelevele  ambayo watoto mnawafundisha mambo yanayowazidi matokeo yake ndo mimba za utotoni,sitaacha kuwakamata na kuwachukulia hatua wazazi pande zote mbili na kijana muhusika tena sasa hivi na binti mwenyewe tutamkamata ,”amesema Waryuba

Wakina mama wa kijiji cha Chihangi  na Namikupa ambao walijitokeza kumsikiliza Dc Waryuba

Aidha amesema Kata ya Namikupa ni miuongoni mwa maeneo ambayo yapo mpakani   wananchi wanatakiwa   kutoa taarifa  kwa mgeni yeyote  ambaye anafika katika maeneo yao ili waweze kumtambua  ili kuendelea kulinda amani,usalama na utulivu

Dc Waryuba (katikati) akimsikiliza  mwananchi wa kijiji cha Milidu akitoa kero yake

“Wilaya yetu ipo mpakani  na nchi ya Msumbiji  hivyo mnatakiwa kutoa taarifa endapo mnaona watu msiowaelewa ili tuchukue hatua za haraka,lakini Wilaya yetu ipo salama tuendelee kuitunza amani na utulivu ambao tunao,na tusikubali kuipoteza amani kwa hali yoyote na tumejipanga kisawasawa,”amesema Waryuba  

Baadhi ya wataalamu wa Halmashauri kutoka idara mbalimbali wakisiliza kwa makini kero za wananchi

Ziara za Dc Wryuba ni muendelezo wa ziara zake za kutembelea vijijini kusikiliza kero za wananchi na kukagua miradi ya maendeleo ambayo inatekelezwa katika maeneo hayo ambapo hadi sasa zaidi ya vijiji 137 kati ya 143  ameweza kuvifikia na vitongoji zaidi ya 50 kati ya 73 vya Mji mdogo Mahuta na Tandahimba ameweza kuvifikia

Matangazo

  • TANGAZO LA WALIOFAULU USAILI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. January 15, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI November 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MKATABA January 08, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MKIMBIZA MWENGE KIWILAYA March 30, 2024
  • Soma

Habari mpya

  • DC MNTENJELE AKABIDHI VISHIKWAMBI KWA MAAFISA UGANI TANDAHIMBA

    February 18, 2025
  • KU WILAYA YA TANDAHIMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU MWAKA 2025

    February 17, 2025
  • Vipaumbele Mahususi vya Bajeti ya 2025/2026 Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba.

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI TANDAHIMBA LAPITISHA MAKISIO YA MPANGO NA BAJETI YA TSH .BIL.40.2 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026.

    February 13, 2025
  • Soma

Video

MKUU WA WILAYA YA TANDAHIMBA PAMOJA NA MKURUGENZI WASHIRIKI UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAHEHA
Video nyingin

Kurasa za karibu

  • Ijue Tandahimba.

Viungio vinavyousiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • President's Official Website
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya sehemu

Tandahimba District Council

Wasiliana Nasi

    TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA

    Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA

    Simu: +25523 2410030

    Simu:

    Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa