• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
Tandahimba District Council
Tandahimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Idara na Vitengo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Kumuona Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoko kwenye Mpango
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Zabuni
    • Kanuni na Taratifbu
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha habari
    • Habari Mpya
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya picha

Dc Waryuba awataka maafisa ugani wa vijiji na kata kuwa na mashamba ya mfano

Posted on: January 6th, 2021

Na Kitengo cha Habari na Mawasiliano

Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Sebastian Waryuba amewataka maafisa ugani kuwa karibu na wakulima katika maeneo yao kwa kuwapa ushauri wa kilimo ili kuongeza uzalishaji wa zao la korosho na mazao mengine ya chakula

Ameyasema hayo wakati akifungua mkutano wa maafisa ugani wa  Vijiji na Kata jana katika ukumbi wa mikutano,amesema pamoja na kutoa ushauri maafisa ugani katika maeneo yao wanapaswa kuwa na mashamba ya mfano ili wakulima wajifunze kutoka kwao

Maafisa Ugani wa kata na vijiji  kwenye mkutano  wa kupanga mikakati ya kuleta mapinduzi ya uzalishaji

Amesema  kuwa  ili kuweza kuongeza uzalishaji ni jukumu la maafisa ugani  kuhamasisha wakulima kutibua mashamba ya korosho ili maji yaweze kuingia kwenye ardhi  sambasamba na kuondoa mikorosho iliyozeeka kwa kusimamia ukataji wa kitaalam

Dc Waryuba akiwasistizia maafisa ugani kusimamia kampeni ya ondoa mapori ongeza uzalishaji

“Mikorosho inahitaji maji ya kutosha wahamasisheni wakulima watibue mashamba yao ili maji yaweze kuingia kwa wingi katika mikorosho ili tuongeze uzalishaji na hiki kipindi cha mvua tusisahau mazao mengine wananchi walime mazao ya chakula,hatutaki njaa katika Wilaya yetu,”amesema Dc Waryuba


Mkurugenzi Mtendaji ndg Said Msomoka (kati) akiwa na Mweka hazina   Ally Machela(kushoto) na Afisa Kilimo  Issa  Naumanga kwenye Mkutano  na maafisa Ugani wa kata na vijiji

Naye Mkurugenzi Mtendaji  wa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba ndugu Said Msomoka amesema kampeni ya ondoa mapori ongeza uzalishaji italeta mapinduzi katika Halmashauri kwakuwa wakulima wapo tayari kuondoa mikorosho iliyozeeka

Mkurugenzi Mtendaji ndg Said Msomoka akieleza jambo kwa maafisa  ugani

“Hii kampeni  italeta mapinduzi makubwa katika uzalishaji lakini maafisa ugani  wakulima wanawategemea kitaalam nendeni mashambani walipo  ili turudi tulipo kiuzalishaji naamini tunaweza tukisimama kila mmoja sehemu yake,”amesema Mkurugenzi

 

Matangazo

  • TANGAZO LA WALIOFAULU USAILI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. January 15, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI November 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MKATABA January 08, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MKIMBIZA MWENGE KIWILAYA March 30, 2024
  • Soma

Habari mpya

  • DC MNTENJELE AKABIDHI VISHIKWAMBI KWA MAAFISA UGANI TANDAHIMBA

    February 18, 2025
  • KU WILAYA YA TANDAHIMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU MWAKA 2025

    February 17, 2025
  • Vipaumbele Mahususi vya Bajeti ya 2025/2026 Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba.

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI TANDAHIMBA LAPITISHA MAKISIO YA MPANGO NA BAJETI YA TSH .BIL.40.2 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026.

    February 13, 2025
  • Soma

Video

MKUU WA WILAYA YA TANDAHIMBA PAMOJA NA MKURUGENZI WASHIRIKI UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAHEHA
Video nyingin

Kurasa za karibu

  • Ijue Tandahimba.

Viungio vinavyousiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • President's Official Website
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya sehemu

Tandahimba District Council

Wasiliana Nasi

    TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA

    Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA

    Simu: +25523 2410030

    Simu:

    Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa