• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
Tandahimba District Council
Tandahimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Idara na Vitengo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Kumuona Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoko kwenye Mpango
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Zabuni
    • Kanuni na Taratifbu
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha habari
    • Habari Mpya
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya picha

Dc Sawala apiga marufuku ngoma za usiku Wilaya ya Tandahimba

Posted on: November 16th, 2021

 Na Kitengo cha Habari na Mawasiliano 

Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Mhe.Kanali Patrick Sawala amepiga marufuku  ngoma za usiku  na kueleza kuwa zinachangia wanafunzi kupata ujauzito kabla ya wakati wao na kushindwa kuendelea na masomo

Ameyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati akizungumza  na wananchi wa kata ya Mihambwe na  amesema kuwa jukumu la wazazai ni kuhakikisha wanafunzi wanahudhuria shule  ili waweze kufikia malengo yao na kutoruhusu  utoro wa reja reja kwa wanafunzi

Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Mhe.Kanali Patrick Sawala akizungumza na wananchi wa Kata ya Mihambwe

“Marufuku ngoma za Usiku kwenye Wilaya ya Tandahimba kwa sasa,sikatazi mila na desturi ila usiku hapana,kwakuwa wanafunzi wetu wanapata jauzito huko kwenye ngoma ngoma ambapo wanakutana na mafataki,tena ukibainika umempa mwanafunzi mimba hakuna majadiliano ni  mahakamani sharia inasema kosa hilo ni  miaka thelathini  jela tena mimi natamani wangechapwa na viboko,kwakuwa wanakatisha ndoto za wanafunzi wetu,”amesema Dc Sawala

Aidha Dc Sawala katika mkutano huo amewasistiza wananchi kuendelea kuimarisha  ulinzi  na usalama  katika maeneo yao,kuendelea kuchukua hatua dhidi ya UVIKO-19  na kupata chanjo ambayo inapatikana katika vituo vya serikali, kulima mazao mchanganyiko na kuongeza jitihada  zao la ufuta  ili kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja lakini pia Taifa kwa ujumla

 Wananchi wa kata ya Mihambwe wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Mhe.Kanali Sawala (Hayupo Pichani)

“Nawapongeza wananchi kwa jinsi ambavyo mnashirikiana kuhakikisha ulinzi na usalama unaimarika,lakini pia naendelea kusistiza kuwa kila mgeni anayekuja katika kijiji taarifa zake zichukuliwe kwenye madaftari ya wakazi  ambayo yapo kuanzia ngazi ya vijiji na vitongoji,”amesema Dc Sawala

Naye Mkurugenzi Mtendaji  Halmasahauri ya Wilaya ya Tandahimba ndugu Mussa Gama akizungumza na wananchi wa Kata ya Mihambwe amesema kuwa ushiriki wa wananchi katika miradi ya maendeleo ni muhimu kwakuwa wao ni wahusika wakuu wa miradi hiyo  katika maeneo yao

Mkurugenzi Mtendaji ndg Gama akizungumza na baadhi ya wananchi na kamati ya mradi ambao walifika kushiriki mradi wa vyumba vya madarasa Sekondari ya Michenjele

“Nawaomba mshiriki katika miradi hii ya madarasa na vituo vya afya ,fedha ipo lakini mkishiriki gharama ambazo zingetakiwa kulipwa zinabaki kwenye kijiji kwaiyo kituo kikikamlika zile fedha zinaweza kutumika kwa kuongeza dawa au kujenga nyumba ya m ganga,”amesema Mkurugenzi 

 

 Mkurugenzi Mtendaji ndg Gama  akijitambulisha kwa wananchi wa kata ya Mihambwe

   

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 05, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI November 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MKATABA January 08, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MKIMBIZA MWENGE KIWILAYA March 30, 2024
  • Soma

Habari mpya

  • DC MNTENJELE AKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO SEKTA YA ELIMU

    June 25, 2025
  • DED MWANZALIMA ATEMBELEA MIRADI YA ELIMU

    June 21, 2025
  • TANDAHIMBA YAPATA HATI SAFI MARA YA TANO MFULULIZO.

    June 17, 2025
  • WAZIRI SIMBACHAWENE AMPONGEZA MKURUGENZI WA TANDAHIMBA NA MADIWANI KWA KUFANYA ZIARA YA MAFUNZO SIMIYU.

    June 11, 2025
  • Soma

Video

MKUU WA WILAYA YA TANDAHIMBA PAMOJA NA MKURUGENZI WASHIRIKI UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAHEHA
Video nyingin

Kurasa za karibu

  • Ijue Tandahimba.

Viungio vinavyousiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • President's Official Website
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya sehemu

Tandahimba District Council

Wasiliana Nasi

    TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA

    Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA

    Simu: +25523 2410030

    Simu:

    Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa