• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
Tandahimba District Council
Tandahimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Idara na Vitengo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Kumuona Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoko kwenye Mpango
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Zabuni
    • Kanuni na Taratifbu
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha habari
    • Habari Mpya
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya picha

Dc Sawala aagiza utaratibu wa kuwapima ujauzito wanafunzi wa kike uanze rasmi

Posted on: September 9th, 2021

Na Kitengo cha Habari na Mawasilano

Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Mhe.Kanali  Patrick Sawala  amesema utaratibu wa kuwapima wanafunzi wa kike ujauzito uanze rasmi katika  shule zote ndani ya Wilaya

Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Kanali Patrick Sawala akizungumza kwenye kikao cha baraza la madiwani

Ameyasema hayo jana Septemba 7,2021 kwenye kikao cha kawaida cha baraza la madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Tandahimba

Madiwani wakiwa kwenye  kikao

“Naagiza rasmi utaratibu wa kuwapima mimba watoto wakike uanze rasmi katika shule zetu zote ndani ya Wilaya lakini natoa wito wazazi  na walezi kutoa ushirikiano mara inapobainika mwanafunzi amepewa mimba  ili hatua za kisheria zichukue mkondo wake,”amesema Dc Sawala

Wakuu wa Idara na Vitengo wakiwa kwenye kikao cha baraza la madiwani

Aidha katika taarifa yake ameelezea masuala mbalimbali ikiwemo afya,elimu,kilimo na ushirika,ulinzi na usalama,maji,usimamizi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayoendelea katika maeneo mbalimbali ndani ya Wilaya

Kamati ya Ulinzi na usalama  wakiwa kwenye kikao cha baraza la madiwani

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba Ndugu Mussa Gama akijibu swali la papo kwa papo la Mhe.Njawala Njawala diwani wa kata ya  Mnyawa,amesema Halmashauri imejipanga kusimamia na kutekeleza miradi kwa wakati

Mkurugenzi Mtendaji ndg Mussa Gama akijibu swali la papo kwa papo  kutoka kwa madiwani

“Nikuondoe hofu Mhe. Njawala mimi na timu yangu tumejipanga kuisimamia miradi inayotekelezwa kuwa inakamilika kwa wakati ili wananchi wapate huduma,”amesema ndg Gama

Aidha naye Meneja Wakala wa Barabara Vijijini (Tarura) Wilaya ya Tandahimba Mhandisi Peter Mliya  amewaomba madiwani kuwa wavumilivu ili fedha iliyopatikana ipelekwe katika maeneo ambayo tayari yapo kwenye mpango 

Meneja wa Tarura Wilaya ya Tandahimba Mhandisi Peter Mliya akijibu maswali ya madiwani ya papo kwa papo

“Nafahamu kuna barabara korofi lakini wananchi wasichote mchanga barabarani kwakuwa wanasababisha mashimo na kuzidisha ubovu,tutakarabati baadhi lakini tuna mpango wa kujenga  barabara km 4 kwa lami,barabara zingine tutaziweka kwenye bajeti ijayo,”amesema Mhandisi

Viongozi wa vyama vya siasa wakifuatilia kikao cha baraza la madiwani

Matangazo

  • TANGAZO LA WALIOFAULU USAILI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. January 15, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI November 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MKATABA January 08, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MKIMBIZA MWENGE KIWILAYA March 30, 2024
  • Soma

Habari mpya

  • DC MNTENJELE AKABIDHI VISHIKWAMBI KWA MAAFISA UGANI TANDAHIMBA

    February 18, 2025
  • KU WILAYA YA TANDAHIMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU MWAKA 2025

    February 17, 2025
  • Vipaumbele Mahususi vya Bajeti ya 2025/2026 Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba.

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI TANDAHIMBA LAPITISHA MAKISIO YA MPANGO NA BAJETI YA TSH .BIL.40.2 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026.

    February 13, 2025
  • Soma

Video

MKUU WA WILAYA YA TANDAHIMBA PAMOJA NA MKURUGENZI WASHIRIKI UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAHEHA
Video nyingin

Kurasa za karibu

  • Ijue Tandahimba.

Viungio vinavyousiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • President's Official Website
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya sehemu

Tandahimba District Council

Wasiliana Nasi

    TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA

    Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA

    Simu: +25523 2410030

    Simu:

    Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa