Na Kitengo cha Habari na Mawasiliano
Wakuu wa Idara na vitengo (CMT) Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba wamepewa mafunzo ya jinsi ya kutumia mfumo wa e-Mrejesho ili kujibu malalamiko ya watumishi na wananchi ambayo yatahusu idara husika kwa wakati
Wakuu wa Idara na Vitengo (CMT) wakifuatilia mafunzo hayo
Akielezea mfumo huo kwa CMT leo Juni 30,2022 katika ukumbi wa mikutano wa Halmasahauri,Afisa Malalamiko Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba Bi.Judicy Mnzava amesema kuwa mfumo huo utarahisisha malalamiko kujibiwa kwa wakati
Bi.Judicy Mnzava Afisa Malalamiko akielezea mfumo wab e-Mrejesho jinsi unavyoweza kurahisisha huduma kwa wananchi
“Mfumo huu lengo ni kurahisisha huduma kwa mteja ambaye ni mwananchi hivyo utawawezesha CMT kujibu malalamiko ambayo yatahusu idara zao kuyashughulikia kwa wakati na mwananchi au mtumishi atayapata majibu ya malalamiko yake eneo lolote alilopo kwa njia ya simu au kama ametumia mtandao wa tovuti atapata majibu,”amesema Bi.Mnzava
Aidha amesema kuwa mfumo huu utapokea malalamiko lakini mwananchi anaweza kutuma pongezi na maoni yake bila kufika Halmashauri na yatashughulikiwa na majibu yatamfikia kwa wakati
Naye Ndugu. Issa Naumanga Mkuu wa Idara ya Kilimo na Ushirika amesema mfumo huo utaongeza uwajibikaji katika kushughulikia malalammiko ambayo yatatolewa na watumishi na wananchi
TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA
Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA
Simu: +25523 2410030
Simu:
Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz
Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa