• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
Tandahimba District Council
Tandahimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Idara na Vitengo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Kumuona Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoko kwenye Mpango
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Zabuni
    • Kanuni na Taratifbu
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha habari
    • Habari Mpya
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya picha

ATAKAYEUZA PEMBEJEO KIHOLELA MITAANI KUKIONA CHA MOTO

Posted on: August 19th, 2021

Na Kitengo cha Habari na Mawasiliano

Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Mhe Kanali Patrick Sawala amewataka wakulima kununua pembejeo katika maduka rasmi ili kuepuka  kupata pembejeo  ambazo zinawea kuleta madhara  kwenye mikorosho

Dc Sawala akiongea na wananchi wa Kata ya Kitama

Ameyasistiza hayo kwa nyakati tofauti akiwa pamoja na Mbunge wa Jimbo la Tandahimba Mhe. Katani Katani na Wakuu wa Idara  kwenye ziara zake za kujitambulisha na kusikiliza kero za wananchi  katika  kata ya Miuta na Kitama ambapo amewatahadhalisha kuwa makini na wauzaji holela wa viuatilifu wanaopita  katika mitaa na vijiji

Wananchi wa kata ya Kitama wakimsikiliza  Mkuu wa Wilaya (Hayupo pichani)

“Kuna uuzaji holela wa viuatilifu katika maeneo mbalimbali unafanywa na watu wasio waaminifu ,wakulima msinunue nendeni mkanunue kwenye maduka rasmi ambayo yanauza pembejeo endapo kuna tatizo ni rahisi kufuatilia kuliko hao wapita njia na tukiwakamata tutawachukulia hatua kali,”amesema Dc Sawala

Dc Sawala akiongea na wananchi wa kata ya Miuta

Aidha amesema pembejeo ambazo zimetolewa na  serikali kwa wakulima zinaendelea kusambazwa katika vyama vya msingi (amcos) kwa usimamizi maalumu ili  wakulima waweze kunufaika na pembejeo hizo

Dc Sawala (kushoto) akimsikiliza katibu wa Amcos ya Dinyanga iliyopo kata ya  Kitama kuhusu ugawaji wa pembejeo katika amcos hiyo

“Sasa hivi nimeweka utaratibu maalum katika ugawaji wa pembejeo hizi,kwaiyo itagawiwa kwa wakulima kwa kufuata haki na utaratibu ili wakulima wanufaike na pembejeo hizi,na ninapita mwenyewe kwa baadhi ya amcos ili kujiridhisha endapo zoezi hili linafanyika kwa kuzingatia haki,”amesema Dc Sawala

Baadhi ya wakuu wa idara  na vitengo wakifuatilia mkutano huo

Naye Mbunge Wa Jimbo la Tandahimba Mhe.Katani amesema ataendelea kusimamia  ili thamani ya zao la korosho ya Tandahimba iendelee kubaki kuwa juu  kwasababu ndiyo wazalishaji wakubwa wa zao hilo na hawana historia ya kuwa na  korosho mbovu

Mbunge wa Jimbo la Tandahimba Mhe. katani akisema neno kwa wananchi wa kata ya Miuta

Katika ziara  zake Dc Sawala ameendelea kuwasistiza wazazi kuhakikisha watoto wanahudhuria shule kutokomeza vitendo vya utoro na mimba mashuleni,wananchi kuendelea kuzingatia maelekezo yanayotolewa na idara ya afya kuhusu  UVIKO-19,kushiriki katika miradi ya maendeleo,kuendelea kulinda amani na utulivu ndani ya wilaya  sambamba na watendaji kupata taarifa za wageni wanaofika katika maeneo yao kwa kuwaoredhesha kwenye vitabu vyao vya wakazi

Wananchi wa Kata ya Miuta wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya Kanali Sawala

Matangazo

  • TANGAZO LA WALIOFAULU USAILI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. January 15, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI November 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MKATABA January 08, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MKIMBIZA MWENGE KIWILAYA March 30, 2024
  • Soma

Habari mpya

  • DC MNTENJELE AKABIDHI VISHIKWAMBI KWA MAAFISA UGANI TANDAHIMBA

    February 18, 2025
  • KU WILAYA YA TANDAHIMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU MWAKA 2025

    February 17, 2025
  • Vipaumbele Mahususi vya Bajeti ya 2025/2026 Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba.

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI TANDAHIMBA LAPITISHA MAKISIO YA MPANGO NA BAJETI YA TSH .BIL.40.2 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026.

    February 13, 2025
  • Soma

Video

MKUU WA WILAYA YA TANDAHIMBA PAMOJA NA MKURUGENZI WASHIRIKI UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAHEHA
Video nyingin

Kurasa za karibu

  • Ijue Tandahimba.

Viungio vinavyousiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • President's Official Website
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya sehemu

Tandahimba District Council

Wasiliana Nasi

    TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA

    Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA

    Simu: +25523 2410030

    Simu:

    Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa