• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
Tandahimba District Council
Tandahimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Idara na Vitengo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Kumuona Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoko kwenye Mpango
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Zabuni
    • Kanuni na Taratifbu
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha habari
    • Habari Mpya
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya picha

Dc Waryuba : Ni wajibu wa wazazi , walezi na jamii kuwalinda na kuwatetea watoto

Posted on: June 18th, 2021

Na Kitengo cha Habari na Mawasilano

Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Mhe.Sebasian Waryuba amesema  wazazi , walezi na jamii kwa ujumla wana wajibu wa kuwatunza watoto na kuwapatia mahitaji muhimu sambamba na kuwalinda na vitendo vya kikatili ambavyo vinaweza kuwapata katika maeneo yao

Watoto nawazazi ambao wamehudhuria katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika kijiji cha Mitondi B

Ameyasema hayo kwenye siku ya maadhimisho ya mtoto wa afrika yenye kauli mbiu ya "Tutekeleze ajenda 2040: kwa Afrika inayolinda haki za watoto" ambayo Kiwilaya yamefanyika katika  kijiji cha Mitondi B kata ya Kitama,  Dc Waryuba akiwa ameambatana na Mkurugenzi Mtendaji,kamati ya Ulinzi naUsalama na wakuu wa idara na viteng alianza kwa kupokea maandamano ya watoto waliobeba mabango yenye jumbe mbalimbali

Dc Waryuba akisistiza umuhimu wa kuwalinda watoto katika jamii kwenye maadhimisho hayo

 “Watoto hawa wana haki ya kupata elimu,afya bora,chakula,kutetewa,kuwalinda,kuwatunza  ,wajibu wa mzazi na mlezi ni wa kudumu  kuhakikisha mtoto anapata haki zake,wazazi mzingatie watoto wanahudhuria shule wasiwe watoro wa shule  ,”amesema Dc Waryuba

Dc Waryuba (aliyesimama) akizungumza na wananchi wa Mitondi B

Aidha naye  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmasahauri ya Wilaya ya Tandahimba Ndg Said Msomoka akitolea majibu ya changamoto ambazo zimetolewa na mwenyekiti wa kijiji hicho ya zahanati na  uhaba wa walimu amesema kuwa kwa mwaka unaokuja zahanati imetengewa Mil 40 ambazo zitakuja kufanya kazi ili watoto na jamii kwa ujumla wapate huduma stahiki

Mkurugenzi Mtendaji ndg Said Msomoka akitoa neno kwenye maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika

“ Kwa mwaka huu wa fedha unaoanza mwezi ujao  zimetengwa mil 40 lakini tutajitahidi tufanye haraka ili huduma za  wagonjwa wa nje  zianze mapema kwa suala la uhaba wa walimu tumelichukua,”amesema ndg Msomoka

Kamati ya Ulinzi na usalama na wakuu wa idara na vitengo ambao pia walihuduruia maadhimisho hayo

Aidha katika maadhimisho hayo Dc Waryuba alikabidhi  taulo za kike kwa mratibu wa elimu kata  na matroni  ambazo zilitolewa a taasisi ya Search for Common Ground ambayo imetoa taulo 1000 na shirika la Sports Development Aid wametoa taulo 60 za kike na kusistiza kuwa taulo hizo ziwafikie wahusika

Maadhimisho ya mtoto wa Afrika Wilaya ya Tandahimba yamelenga  kuhamasisha  jamii kuhusu umuhimu wa masuala ya kupinga ukatili  dhidi ya watoto lengo ni kuhakikisha watoto wanakuwa salama kuanzia ngazi ya Familia kijiji,kata na Wilaya na kupambwa na burudani mbalimbali

           Igizo la bunge la watoto


Wanafunzi wakiimba ngonjela kwenye maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika kijiji cha Mitondi B

Matangazo

  • TANGAZO LA WALIOFAULU USAILI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. January 15, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI November 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MKATABA January 08, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MKIMBIZA MWENGE KIWILAYA March 30, 2024
  • Soma

Habari mpya

  • DC MNTENJELE AKABIDHI VISHIKWAMBI KWA MAAFISA UGANI TANDAHIMBA

    February 18, 2025
  • KU WILAYA YA TANDAHIMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU MWAKA 2025

    February 17, 2025
  • Vipaumbele Mahususi vya Bajeti ya 2025/2026 Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba.

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI TANDAHIMBA LAPITISHA MAKISIO YA MPANGO NA BAJETI YA TSH .BIL.40.2 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026.

    February 13, 2025
  • Soma

Video

MKUU WA WILAYA YA TANDAHIMBA PAMOJA NA MKURUGENZI WASHIRIKI UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAHEHA
Video nyingin

Kurasa za karibu

  • Ijue Tandahimba.

Viungio vinavyousiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • President's Official Website
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya sehemu

Tandahimba District Council

Wasiliana Nasi

    TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA

    Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA

    Simu: +25523 2410030

    Simu:

    Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa