• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
Tandahimba District Council
Tandahimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Idara na Vitengo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Kumuona Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoko kwenye Mpango
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Zabuni
    • Kanuni na Taratifbu
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha habari
    • Habari Mpya
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya picha

Huduma za afya

Huduma za Afya

Wilaya ya Tanndahimba ina jumla ya vituo 34 vya kutolea huduma za afya. Hii ni pamoja na Hospitali moja inayomilikiwa na  serikali, vituo vya afya 3 kimoja kati ya vituo hivyo kinamilikiwa na  shirika la Kanisa la Katoliki na  vituo vingine  2 vinamilikiwa na  serikali.Pia  kuna zahanati 30, zahanati 29  kati ya hizo  zinamilikiwa na serikali na  moja inamilikiwa na  mtu binafsi. Pia kuna maduka ya dawa  baridi 27.


HUDUMA ZA UCHUNGUZI

Katika kuendeleza na kufuata kanuni za utoaji wa huduma bora za afya , hospitali imekuwa ikitoa huduma za uchunguzi wa magonjwa mbalimbali kabla ya mgonjwa kuanzishiwa matibabu. Huduma hizo za uchunguzi zinafanywa kupitia maabara iliyopo ambayo ina uwezo wa kufanya uchunguzi wa takribani vipimo vyote vya msingi , kwa kipindi cha mwezi January-December 2016 vipimo mbalimbali vilifanyika kama inavyoonyesha kwenye jedwali hapo chini

KIPIMO
Extremities
Chest x-ray
Pelvis
Skull
 Cervical Spine
Lumber Spine
Thoracic/Spine
Lumber Sacral
Abdominal X – ray
Barium Swallow
Barium meal
Obstretic ultrasound
Intravenous Urography
Hystero Salpingograph

HUDUMA ZA DAMU SALAMA

Hospitali inatoa huduma za upasuaji hata hivyo katika kuboresha huduma za dharura kwa wagonjwa wanaohitaji damu wakati wa upasuaji pamoja na wagonjwa wenye upungufu wa damu, hospitali inaendesha zoezi la ukusanyaji damu na kuanzia mwezi may 2016 jumla ya sampuli 846 za damu zilikusanywa. Kati ya hizo units 751 zimetumika.

Zoezi la ukusanyaji damu linakabiliwa na changamoto za mara kwa mara za upatikanaji  wa mifuko ya kuhifadhia damu pia mwamko mdogo katika uchangiaji toka kwenye jamii

Huduma za uzazi na watoto

Katika kuboresha huduma kwa wajawazito halmashauri imekuwa ikiendelea kutoa  huduma za chanjo, upimaji wa wingi wa damu  pamoja na kutoa elimu kwa wajawazito juu ya  utambuzi wa dalili hatari kwa mjamzito pamoja na kusisitiza wajawazito kuwahi kliniki na kujifungulia katika vituo vya huduma za afya. Aidha halmashauri imeendelea kufutailia uwepo wa dawa muhimu kwa wajawazito wakati wa kujifungua ikiwemo dawa za Oxtocin na Magnesium Sulphate. Pia halmashauri inatoa huduma za upasuaji wa dharura kwa akina mama wajawazito katika vituo vya afya viwili na hospitali moja.

Mapambano dhidi ya ukimwi

Mapambano dhidi ya ugonjwa wa UKIMWI ni kipaumbele kimojawapo halmashauri ina jumla ya vituo 33 vinavyotoa dawa za kufubaza VVU kwa wananchi wanaoishi na VVU. Aidha katika maambukizi mapya Halmashauri imekuwa ikiendelea kutoa elimu kwa wananchi jinsi ya kujikinga na maambukizi ya VVU. Hata hivyo kwa upande wa watumishi imekuwa ikihakikisha kuwepo kwa vifaa vya kusaidia kuwakinga watumishi wakati wa kutoa huduma kwa wagonjwa. Aidha halmashauri bado imekuwa ikiendelea kuendesha vikao na   kutoa elimu kwa vikundi vya kina mama wajawazito wanaoishi na VVU kwa lengo la kuwakinga watoto wasizaliwe na VVU. Pia halmashauri kwa kupitia vituo vyake 12 vya huduma za afya vimekuwa ikiendelea kutoa huduma ya kupima kinga za mwili (CD-4) kwa wananchi wanaoishi na VVU kila baada ya miezi sita pamoja na kuchukua damu za watoto waliozaliwa na kina mama wenye VVU kwa ajili ya upimaji wa VVU. Hadi sasa jumla ya wanaoishi na virusi vya ukimwi ni 5,081 kati yao wanaume ni 1,655 na wanawake ni 3,426.Mammbukizi ya ukimwi kwa sasa ni 3% katika wilaya.

HUDUMA ZA MAABARA.

VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA:

Halmashauri ina jumla ya vituo 4 vya kutolea huduma za maabara katika vituo hivyo Hospitali 1inayomilikiwa na Serikali.Vituo vya Afya 3 kimoja kati ya hivyo kinamilikiwa na shirika la Dini.Vituo vingine 2 vinamilikiwa na Serikali.

VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA:

JINA LA KITUO
AINA KITUO
MMILIKI
TANDAHIMBA HOSPITALI
HOSPITALI
SERIKALI
NAMIKUPA
KITUO CHA AFYA
SERIKALI
MAHUTA
KITUO CHA AFYA
SERIKALI
LUAGALA
KITUO CHA AFYA
SHIRIKA LA DINI


HUDUMA ZA MAABARA ZINAZOTOLEWA HOSPITALI YA WILAYA

>Upimaji wa kinga mwili (CD4 Testing)

>Upimaji wa Vikope vya VVU kwenye Damu (Viral Load)

>Huduma ya Daamu Salama (Blood Transfusion)

>Upimaji wa makundi ya damu na Compatibility Test.

>Upimaji wa uwingi wa Damu (HB)

>Upimaji wa MALARIA.

>Upimaji wa Sukari kwenye Damu

>Upimaji wa Kaswende kwenye Damu

>Upimaji wa CHOO haja Kubwa

>Upimaji wa MKOJO

>Upimaji wa makohozi (TB).

>Upimaji wa PITC

>FBP

>S.CREATININE na ALAT/ASAT

HUDUMA YA DAMU SALAMA.

Banki  ya Damu ya Hospitali ya Wilaya inapata Damu kwa njia Uchangiaji damu wa hiari.

MAENEO YA UCHNGIAJI DAMU:

>Shule za Sekondari.

>Taasisi za Dini (Kanisani& Misikitini) na

>Viwandani.

Sampuli za Damu hupelekwa  Banki ya Damu ya Kanda ya Kusini (SZBTS) MTWARA.

Sampuli za Damu huchunguzwa magonjwaa makubwa manne.(Four Markers)

>HIV

>HBV

>HCV na

>KASWENDE (Syphilis)

Mwaka 2016 Jumla ya chupa 846 za Damu zilikusanywa.

Sampuli 95 Zilionekana kuwa na maambukizi mbalimbali:

>HIV sampuli 27= (3.19%)

>HBV Sampuli 35= (4,1%)

>HCV Sampuli 8=(0.9%)

>SYPHILIS Sampuli 25 =(2,9%)

VIPIMO VYA MALARI 2016:

Jumla ya Vipimo vyote vya malaria
42039
Positive Malaria
16701

VIPIMO VYA WEKUNDU WA DAMU:

Jumla ya vipimo vyote vya HB
7116
HB chini ya 70g/L(5O%)
925

VIPIMO VYA KASWENDE:

Jumla ya vipimo vyoyte vya kaswende
1945
Positve Syphilis
152




VIPIMO VYA SUKARI KWENYE DAMU:

Jumla ya vipimo vyote vya sukari
3199
Juu ya 10mmol/L(180mg/L)
589

VIPIMO VYA CHOO( HAJA KUBWA)

Jumla ya vipimo vyote vya choo
1655
Positive H/Worms
41

VIPIMO VYA MKOJO:

Jumla ya vipimo vyote vya mkojo
8025
Posittive S.Haematobium
32

VIPIMO VYA MAKOHOZI:

Jumla ya vipimo vyote vya makohozi
1416
Positive AFB
156



Matangazo

  • Ratiba ya Usafi kila jumamosi ya mwisho wa mwezi. January 03, 2018
  • Siku ya mazoezi kila jumamosi ya pili ya mwezi January 03, 2018
  • TANGAZO LA UJIO WA MWENGE WA UHURU 2018 WILAYANI TANDAHIMBA June 09, 2018
  • Soma

Habari mpya

  • Dc Waryuba : Samani hizi zitawasaidia wanafunzi wetu

    April 01, 2021
  • ZAIDI YA MIL.279 ZATUMIKA MALIPO YA WALENGWA WA TASAF TANDAHIMBA

    April 01, 2021
  • Baraza la madiwani Tandahimba wapitisha Bajeti ya zaidi ya Bil.43.7

    March 09, 2021
  • Mkurugenzi Tandahimba akabidhi vitendea kazi kwa Idara na Vitengo

    February 24, 2021
  • Soma

Video

Byakanwa Afunga mwaka kwa mikakati ya mabadiliko
Video nyingin

Kurasa za karibu

  • Ijue Tandahimba.

Viungio vinavyousiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • President's Official Website
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya sehemu

Tandahimba District Council

Wasiliana Nasi

    TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA

    Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA

    Simu: +25523 2410030

    Simu:

    Barua pepe: ded@tandahimba.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa