• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
Tandahimba District Council
Tandahimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Idara na Vitengo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Kumuona Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoko kwenye Mpango
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Zabuni
    • Kanuni na Taratifbu
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha habari
    • Habari Mpya
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya picha

Idara na Vitengo

IDARA NA VITENGO

1. MIPANGO,TAKWIMU NA UFUATILIAJI

Majukumu ya Idara ya Mipango na Ufuatiliaji ni kama ifuatavyo:-

  1. Uratibu na utayarishaji wa Mpango na Bajeti na kusimamia utekelezaji wake kila mwaka katika Halmashauri.
  2. Kusimamia Uandaaji wa mpango wa utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi kila mwaka.
  3. Kuratibu ufanisi wa mifuko ya Halmashauri: LGCDG, Mfuko wa Jimbo na fedha za mapato ya ndani.
  4. Uratibu na utayarishaji wa Mipango shirikishi katika Kata zote za Halmashauri kupitia Mfumo wa O&OD.
  5. Kusimamia uandaaji wa mipango kazi (Action Plans) ya bajeti za kila mwaka na kuziwasilisha katika ngazi husika..
  6. Kuratibu uandaaji wa maandiko ya miradi mbalimbali ya maendeleo.
  7. Kuratibu maandalizi na utekelezaji wa Mpango wa Matokeo Makubwa sasa (BRN)
  8. Kuratibu maandalizi ya Sera na Mpango Mkakati wa Halmashauri
  9. Kuratibu uandaaji wa taarifa mbalimbali za Halmashauri pamoja na taarifa za utekelezaji wa maagizo kutoka mamlaka za juu za serikali

2.ELIMU YA MSINGI

MAJUKUMU YA IDARA ELIMU MSINGI

1.Kuratibu mitihani ya ndani na nje ya wilaya

2.Kufanya tathimini ya mitihani mbalimbali

3.Kusimamia usajili wa wanafunzi

4.Kuratibu elimu msingi, elimu ya watu wazima na elimu nje ya mfumo rasmi

5.Kuthibiti takwimu za wanafunzi,walimu,majengo na samani

6.Kusimamia taaluma katika wilaya

7.Kufanya tafiti mbalimbali za kielimu

8.Kusimamia uboreshaji wa mazingira ya shule

9.Kusimamia elimu ya kujitegemea na lishe shuleni

10.Kusimamia miradi ya maendeleo iliyoelekezwa shuleni

11.Kusimamia matumizi ya fedha za ruzuku za uendeshaji shuleni

12.Kuendesha mafunzo mbalimbali ya kuinua taaluma za walimu

13.Kuratibu elimu kwa wanafunzi wenye maalumu

14.Kuratibu na kusimamia vituo vya ufundi stadi

15. Kusimamia na kuratibu michezo na sanaa za maonesho

3 IDARA YA ELIMU SEKONDARI

KAZI KUU ZA IDARA HII.

Kuratibu shughuli zote za matumizi ya fedha za Elimumsingi msingi bila malipo katika shule

Kukusanya, kuchambua na kuwasilisha takwimu muhimu za idara kadiri zinapohitajika.

Kusimamaia utawala bora mashuleni.

Kuandaa taarifa za robo mwaka za utekelezaji wa maendeleo ua elimu na kuwasilisha WEMU na OR- TAMISEMI

Kutoa mapendekezo ya uteuzi wa wakuu wa shule

Kushughulikia uhamisho wa walimu na watumishi wasio walimu na wanafunzi ndani ya Halmashauri

Kutathmini utendaji kazi wa walimu na watumishi wasio walimu

Kusimamia utekelezaji wa taarifa ya ukaguzi wa shule

Kuratibu utekelezaji wa taarifa ya ukaguzi wa shule

Kuratibu na kuendesha vikao vya idara

4.IDARA YA AFYA

1.0 UTANGULIZI: 

Idara ya Afya, imegawanyika katika Vitengo vikuu viwili, ambavyo ni kitengo cha Afya Tiba na Afya Kinga. Aidha idara hii inahudumia wananchi kupitia jumla ya Vituo 36 vya kutolea huduma za Afya.vikiwemo vya Serikali 33, watu Binafsi 3 kama inavyoonekana katika Jedwali hapa chini:-

KITUO CHA HUDUMA
SERIKALI
BINAFSI
MASHIRIKA
JUMLA
Hospitali ya Wiaya
1
0
0
1
Vituo vya Afya
3
0
0
3
Zahanati
29
3
0
32
Jumla:
33
3
0
36

MAJUKUMU YA IDARA YA AFYA

  1. Kuandaa mpango mkakati wa miaka mitano 5 kwa ajili ya uendeshaji wa huduma za afya
  2. Kuandaa bajeti ya mpango kabambe wa afya wa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba.
  3. Kushirikiana na wadau mbalimbali katika kutoa huduma za afya
  4. Kutoa elimu ya afya kinga na Kuzuia magonjwa ya mlipuko
  5. Kufanya usimamizi shirikishi katika vituo vya kutolea huduma za afya
  6. Kutafsiri Sera, Miongozo mbalimbali na viwango vya utoaji huduma kama ilivyowekwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.
  7. Kusimamia matumizi sahihi na mgawanyo wa rasilimali(Rasilimali Watu, Fedha na vitu)
  8. Kuandaa taarifa mbalimbali za utekelezaji wa shughuli za idara ya afya
  9. Kufanya tathimini na tafiti za magonjwa mbalimbali katika Wilaya.
  10. Kushirikiana na Mamlaka ya Chakula na Dawa(TFDA) katika kuhakikisha usalama wa vyakula na dawa kwa Wananchi.
  11. Kufanya ukaguzi na ufuatiliaji wa huduma zinazotolewa na vituo vya kutolea huduma za Afya.
  12. Kutoa Elimu ya lishe bora kwa wananchi.
  13. Kutoa elimu na ushauri katika makundi yanayoishi katika mazingira hatarishi.

5.MAENDELEO YA JAMII, USTAWI WA JAMII NA VIJANA

1.0 UTANGULIZI 

Idara ya Maendeleo ya Jamii inahusika zaidi na kuraghibisha jamii ili iweze kushiriki kikamilifu katika Maendeleo,hii ni pamoja na kubadilisha,mitazamo,fikra,tabia,na mienendo ili iwe chanya kwaajili ya Maendeleo ya wananchi katika Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba.

Kuiwezesha jamii kuibua kupanga na kutekeleza kwa kikamili yale waliyopanga kwa kutumia zaidi raslimali zilizopo maeneo yao na za nje pale zitakapohitajika

Idara ina madawati matano na Kitengo kimoja (1) kama ifuatavyo :

1.MADAWATI:

2.Utafiti na Mipango

3.Dawati la Jinsia na Watoto

4.Kikosi cha Ufundi na Ujenzi

5.Uwezeshaji wananchi kiuchumi

2.VITENGO

1.Idara ina Kitengo kimoja cha vijana

3.0 Pia Idara ina ratibu shughuli zifuatazo

1.Uratibu wa VICOBA

2.Uratibu wa shughuli wa TASAF

3.Uratibu wa Asasi

4.Uratibu wa Shughuli za Mwitiko wa Jamii katika kudhibiti UKIMWI

4.0 MAJUKUMU YA IDARA :

1.Kuhamasisha na kuiwezesha jamii,kushiriki katika kutambua, kuibua, kupanga , kutekeleza, kufuatilia na kutathimini shughuli zao za Maendeleo.(To ensure that community Participate fully in formulating, Planning, implementing and evaluating Development Plans.

2.Kuhamasisha jamii kushiriki katika shughuli zote za Maendeleo ikiwemo miradi ya ujenzi ya kijamii,usafi wa mazingira

3.Kusimamia na kuhamasisha shughuli za uwezeshaji wananchi kiuchumi kupitia vikundi vya uzalishaji mali vya wanawake ,vijana , vikundi vingine vya kiraia

4.Kuratibu shughuli za Mwitiko wa jamii katika kudhibiti UKIMWI

5.Kuhamasisha ujenzi wa nyumba bora na uimarishaji wa vikosi vya ujenzi vya Kata vikiwemo vya vijana

6.Kuhamasisha shughuli zote za Maendeleo ya watoto .

7.Kukusanya takwimu mbalimbali za Maendeleo ya Jamii kwaajili ya Mipango ya Maendeleo ya jamii

8.Kuwezesha wanawake na vijana kuongeza kipato chao kupitia fursa mbalimbali za kiuchumi ikiwemo, utoaji wa mikopo kwa vikundi vya uzalishaji mali vya wanawake na vijana kupitia mfuko wa Maendeleo wa Wanawake na vijana wa Halmashauri

9.Kuratibu shughuli zote za Asasi

10.Kuziwezesha jamii kutambua fursa walizonazo ili kutatua vikwazo vya maendeleo (mipango shirikishi).

11.Kujenga uwezo wa Halmashauri na vijiji juu ya utawala bora, upangaji mipango shirikishi na bajeti.

12.Kueleimisha jamii kuingiza masuala mtambuka katika mipango,bajeti, na shughuli za maendeleo kama usafi wa mazingira, mapambano dhidi ya UKIMWI, Mapambano dhidi ya rushwa na Jinsia

6. KILIMO,UMWAGILIAJI NA USHIRIKA

MAJUKUMU YA IDARA YA KILIMO, UMWAGILIAJI NA USHIRIKA

1.Kutoa ushauri wa kilimo bora katika Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

2.Kusimamia shughuli za kilimo ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba.

3.Kuunganisha wakulima na wadau mbalimbali ndani na nje ya Halmashauri ya wilaya ya Tandahimba

4.Kuunganisha wakulima na masoko ndani na nje ya Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

5.Kuhamasisha uanzishwaji wa vyama vya ushirika ndani ya Halmashauri ya wilaya ya Tandahimba

6.Kutoa elimu ya uendeshaji wa vyama vya ushirika ndani ya Halmashauri ya wilaya ya Tandahimba

7.Kukagua vyama vya ushirika na kutoa ushauri ndani ya Halmashauri ya wilaya ya Tandahimba

8.Kuendeleza kilimo cha umwagiliaji ndani ya Halmashauri ya wilaya ya Tandahimba

9.Kuhakikisha upatikanaji wa pembejeo za kilimo katika Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba.

10.Kutoa taarifa za tahadhari mfano ukame, mafuriko, uwepo wa magonjwa, wadudu na wanyama waharibifu na jinsi ya kukabiliana.

11.Kusimamia na kuhakikisha kuwa miradi ya kilimo inatekelezwa

12.Kuandaa taarifa na kuwasilisha katika mamlaka husika

13.Kuandaa mpango na bajeti ya idara ya Kilimo

14.Kuunganisha wakulima na makampuni yanayouza zana za kilimo

7. MIFUGO NA UVUVI

UTANGULIZI

Idara ya maendeleo ya mifugo na uvuvi inasimamia shughuli zote za ufugaji na uvuvi katika halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba.

MAJUKUMU YA IDARA

  • Kutoa mafunzo/elimu juu ya ufugaji bora na uvuvi,
  • kutoa chanjo za kuzuia magonjwa mbali mbali,
  • usajiri na ufuatiliaji wa mifugo kwa kuweka alama ng’ombe wote.
  • Kuhakikisha usalama wa nyama kwa matumizi ya binadamu
  • Uhimilishaji kwa kutumia mbegu kutoka madume bora
  • Kusimamia raslimali za uvuvi
  • Kusimamia ukusanyaji wa mapato yatokanayo na bidhaa za mifugo na uvuvi
  • Kutoa leseni za uvuvi
  • Kudhibiti uvuvi haramu
  • Kuhamasisha uwekezaji katika sekta ya mifugo na uvuvi
  • Kuunganisha wafugaji na wavuvi na taasisi za utafiti
  • Kuandaa na kuwasilisha taarifa mbalimbali

8. IDARA YA ARDHI

UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YA SEKTA YA ARDHI

 Umilikishaji Ardhi Mjini

Katika mwaka 2016/17 sehemu ya ardhi imeweza kutayarisha hati za kawaida zipatazo 134, inayofanya jumla ya hati kuwa 383.

 Umilikishaji Ardhi Vijijini

Kwa mwaka 2016/17 idara imeweza kuandaa hati 22 kufanya jumla ya hati zote kuwa 4734 za mashamba vilevile utaratibu wauandaaji wa hati za kimila kwa maeneo ya umma na majengo ya serikali yaliyopo vijijini unaendelea.

 Mipango Miji na Upimaji Ramani.

Kwa mwaka 2016/17 idara imeanza kupima eneo la Shule ya msingi Amani na barabara ya mivanga ambapo tunategemea kupima viwanja 200 ambavyo vitauzwa na Halmashauri.

Mchoro wa mipango miji wa kwanza uliandaliwa mwaka 1979 na mpaka sasa tuna michoro ya mipango miji 14 na michoro kumi iko katika matayarisho.

Jedwali na. 1.1:  Michoro ya mipango miji Tandahimba

Na.

Namba ya Mchoro

JIna

Idadi ya viwanja

Viwanja vilivyopimwa

Maelezo

1
52/MT/2/1290
Tandahimba Secondary  School

2

2

Upimaji unaendelea
2
45/7/298
Tandahimba Central area

1030

1030

Upimaji umekamilika
3
45/9/299
Mji Mpya

308

110

Upimaji umekamilika
4
45//TAND/01/600
Central area amendment

176

105

Upimaji umekamilika
5
45/TAND/02/402
Mji Mpya – II

406

55

Upimaji umekamilika
6
45/TAND/03/42002
Mivanga Road Low Density Plots

545

11

Upimaji umekamilika
7
45/TAND/04/112003
Hospital Plot Expansion

129

129

Upimaji umekamilika
8
45/TAND/05/112004
Majengo

88

18

Upimaji umekamilika
9
45/TAND/06/112004
Petrol Station Plot

13

13

Upimaji umekamilika
10
45/07/179A
Amendment of TP Drawing No. 45/07/179

33

33

Upimaji umekamilika
11
03/TAND/14/032015
Proposed Mivanga Road Layout Plan

335

16

Upimaji umekamilika
12
03/TAND/15/032015
Proposed Matogoro Neighborhood Unit Layout

548

45

Upimaji unaendelea
13
03/TAND/16/032014
ProposedSquatter Upgrading At Old Tandahimba – I

247

10

Upimaji unaendelea
14
03/TAND/17/032014
Proposed Mji Mpya Squatter Upgrading - I

419

08

Upimaji unaendelea

Vilevile katika kipindi hiki idara imeanza utaratibu wakuhuisha baadhi ya vijiji na kuwa maeneo ya mpango (Planning Areas) takribani vijiji 44 kutoka kata zote vimependekezwa kuwa maeneo ya mipango ambapo mipango ya kina inaendelea kuandaliwa kadri muda unavyozidi kuendelea na kutokana na mahitaji ya eneo husika. Hii ni kutokana na maagizo ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI) ya kusimamia miji midogo inayoibukia ilikudhibiti uendelezaji holela wa makazi.

 Fidia ya Ardhi na Mimea.

Kwa mwaka 2016/17 idara imelipa fidia za mimea ardhi na usumbufu kwa wananchi takribani 32 ambao wamelipwa kiasi cha Tsh.103,000,000/=, fidia hii inajumuisha eneo la Dampo Mivanga na eneo la Makaburi ya MjiMpya pamoja na maeneo mengine yaliyotwaliwa na Halamashauri tangu mwaka 2011 mpaka 2014.

9. UTUMISHI NA UTAWALA

Idara ya Utawala na Utumishi inashughulikia masuala yote yanayohusu Uendeshaji, Watumishi na Utumishi kama ifuatavyo.

  1. Kuratibu masuala ya Mahusiano na Ustawi wa Wafanyakazi ikiwa na pamoja na masuala ya Afya, Usalama, Michezo na Utamaduni.
  2. Kutoa huduma za Masijala, Ofisi na utunzaji na usimamizi wa kumbukumbu
  3. Kuratibu huduma za Ulinzi, Usafi na utunzaji Ofisi, majengo na maeneo/viwanja vya ofisi na huduma za Usafiri
  4. Kutoa huduma za ujumla za uangalizi wa vifaa vya ofisi na majengo
  5. Kuratibu utekelezaji wa jukumu la kuimarisha Nidhamu ikijumuisha utoaji wa elimu ya kuzuia Rushwa.
  6. Kusimamia hatua/Mchakato wa kuwathibitisha na kuwapandisha vyeo/madaraja watumishi.
  7. Kuwezesha programu za mafunzo elekezi kwa waajiriwa/watumishi wapya
  8. Kusimamia mishahara na kushauri juu ya kusimamia mfumo/orodha ya malipo ya mshahara
  9. Kusimamia utekelezaji wa mfumo wa wazi wa mapitio na upimaji wa utendaji wa kazi (OPRAS)
  10. Kushughulikia na kuhuisha taarifa za watumishi kama Likizo za mwaka, likizo za uzazi na matibab, ruhusa za mafunzo/masomo na watumishi kuondoka kazini
  11. Kuratibu upatikanaji wa mafao ya watumishi (malipo ya pensheni n.k) na madai mengineyo
  12. Kushughulikia upatikanaji wa huduma zinazohusiana na watumishi kuondoka kwenye utumishi (kustaafu, kujiuzulu n.k)
  13. Kusimamia masuala ya kinidhamu

 Kuratibu na kushughulikia malalamiko na mashitaka.

 10. IDARA YA MAJI

1.Huduma mbalimbali zinazotolewa na Idara ya Maji ni:-

  • Upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi wote
  • Jinsi ya kuandaa gharama za mradi wa maji
  • Gharama za kufanya utafiti wa visima virefu
  • Jinsi ya kufanya utafiti wa kujenga mradi wa maji
  • Jinsi ya kufanya usanifu wa miradi ya maji kwa mfumo wa EPANET
  • Jinsi ya kuandaa andiko la miradi ya Maji
  • Taratibu za watu binafsi kuchimba visima virefu na vifupi
  • Taratibu za kuunganishia watu binafsi maji
  • Taratibu za kuwa wakala wa mamlaka ya Maji Makonde
  • Uundaji na usajili wa vyombo vya watumia maji (COWSOs)
  • Mafunzo ya awali ya COWSOs
  • Mafunzo ya usimamamizi wa fedha za maji kwa MFUMO wa MIS
  • Jinsi ya kuandaa bajeti kwa MFUMO wa MTF
  • Taratibu za kuomba VAT Exemption
  • Utaratibu wa kusimamia ujenzi wa miradi mikubwa na midogo
  • Huduma hizi zinatolewaje?
  • Idara inatoa huduma ya maji safi na salama kwa Kujenga na kukarabati miundombinu ya maji
  • Pamoja na Kusimamia vyombo vya watumia maji katika shughuli za uendeshaji na matengenezo ya miradi ya maji Matogoro, Tandahimba, Malamba, Likolombe, Mihambwe, Kitama, Kidoo na Mitondi A
  • Jinsi ya kuandaa gharama za mradi wa maji
  • Gharama hizi huandaliwa baada ya kufanya soroveya ya mradi, na kupata mchuro wa eneo husika, pammoja na idadi ya watu, mifugo, taasisi na viwanda. Pia kujua mradi unatetekelezwa eneo la kijijijni, mji mdogo au miji mikubwa (manispaa, au jiji)
  • Gharama za kufanya utafiti wa visima virefu. 
  • Gharama za visima virefu zinapatikani kwa kufanya utafiti wa awali wa hali ya upatikanaji wa maji (geophysical survey) amabayo inaelekeza hali ya upatikanaji maji sehemu husika, kina cha kuchimba na Njia (method) itakayotumika kwenye uchimbaji. Baada ya taarifa hii gharama za uchimbaji zinaandaliwa.
  • Jinsi ya kufanya utafiti wa kujenga mradi wa maji 
  • Gharama za kujenga mradi wa maji zinapatikana kwanza kwa kujua aina ya chanzo cha maji. Baada ya kujua aina ya chanzo cha maji ndipo soroveya (land surveying) inafanyika ili kujua gharama nyingine za miundombinu ya maji kwa mradi mzima.
  • Jinsi ya kufanya usanifu wa miradi ya maji kwa mfumo wa EPANET
  • Chanzo cha maji kinatakiwa kufahamika (Pumping au Gravity) idadi ya watu, Mwinuko wa njia ya bomba kutoka kwenye chanzo hadi Tanki, pamoja na mfumo wote wa usambazaji maji. Pia kujua matawi ya kusambaza maji kwa mradi mzima na vituo vyake.
  • Jinsi ya kuandaa andiko la miradi ya Maji
  • Chanzo cha maji kinatakiwa kufahamika (Pumping au Gravity) idadi ya watu, Mwinuko wa njia ya bomba kutoka kwenye chanzo hadi Tanki, pamoja na mfumo wote wa usambazaji maji. Pia kujua matawi ya kusambaza maji kwa mradi mzima na vituo vyake. Baada ya hapo unatakiwa kujua andiko hilo linapelekwa wizarani kwa ajili ya fedha au la. Kuna nchi amabazo zina format zao za kuandaa maadiko kulingana na jinsi wanavyotaka. Format hizi zinatofautiana kwa nchi zifuatazo, China, India, Japan, Ufaransa na Ujerman.
  • Taratibu za watu binafsi kuchimba visima virefu na vifupi
  • Utaratibu ni kuwasiliana na ofisi za maji za Bonde la Mto Ruvuma na Pwani ya Kusini, ambao wanatoa kibali cha kuchimba kisima kulingana na mahitaji ya maji unayotaka. Pia wanatoa ushauri kulingana na kiasi cha maji kinachotakiwa na mahitaji ya watu wengine. Baada ya kupata kibali hicho, taratibu za kuwapata wataalamu wa soroveya kwa mteja mwenyewe au kwa kushirikisha ofisi ya Bonde au Maji wilaya. 
  • Taratibu za kuunganishia watu binafsi maji
  • Kama ni Maji kutoka Mamlaka ya Maji Makonde, Mteja anatakiwa kwenda ofisi ya maji Makonde Tandahimba na kupewa maelekezo ya jinsi ya kuomba maji.
  • Kama ni Maji ya Kutoka kwenye COWSOs/ jumuiya za watumia maji, mteja anatakiwa kutembelea ofisi za COWSO ya mradi husoka na kupewa maelekezo ya jinsi ya kuunganishiwa maji.
  • Taratibu za kuwa wakala wa mamlaka ya Maji Makonde
  • Mteja anatakiwa kwenda ofisi ya maji Makonde Tandahimba na kupewa maelekezo ya jinsi ya kuomba maji. Mojawapo ya Taarifa muhimu kuwa nayo ni barua ya kuomba uwakala wa kuuza maji kwenye kituo cha maji iliyopitishwa na serikali ya mtaa au mwenyekiti wa kitongoji. Barua hiyo inakuwa na utambulisho wa mwombaji. Baada ya hapo mteja anapewa maelekezo mengine ya jinsi ya kulipia na kujiunga.
  • Uundaji na usajili wa vyombo vya watumia maji (COWSOs) 
  • Uundaji na usajili wa COWSO/ jumuiya ya watumia maji unafanyika kwa kukutana na wanajamii wenye mradi na kuwaelekeza matakwa ya sera ya maji juu ya uendeshaji na matengenezo. Miradi hii inatakiwa kusimamia na watumia maji wenyewe na wanasimamiwa na serikali za vijiji, kata, Tarafa  na halmashauri kupitia (kupitia idara ya Maji) Jamii husika inatakiwa kuteuwa wawkilishi wake kupitia vituo vya watumia maji au vitongoji au mitaa. Wawakilishi hawa nao hukutana na kuchagua kamati ya uendeshaji ya watu kati ya 8 hadi 12. Kati ya wachaguliwa wanatakiwa pia wawakilishi wa vituo pia huchagua mwenyekiti, Makamu mwenyekiti, Katibu na mweka hazina. Kamati ya uendeshaji hufanya kazi za kila siku za ueneshaji wa mradi.
  • Mafunzo ya awali ya COWSOs
  • COWSOs hizi hupewa mafunzo ya awali ya uendeshaji wa mradi ambayo ni jinsi ya kusoma mita, jinsi ya kupokea fedha, kuzitunza benki, jinsi ya kufanya malipo halali, jinsi ya kuendesha mradi na kusimamia wauza maji. Huelekezwa matumizi ya fedha ambayo ni batili na pia jinsi ya kuendesha vikao vya kila mwezi, miezi mitatu na Mwaka au nusu mwaka
  • Mafunzo ya usimamamizi wa fedha za maji kwa MFUMO wa MIS.
  • Mafunzo ya MIS ni mfumo wa usimamizi wa fedha unaotumiwa na wizara ya maji na umwagiliaji. Mhandisi wa maji anakuwa na neon lake la siri la kuingia na Mhasibu wa maji pia. Maneneo haya ni tofauti kwa sababu kila mmoja ana maeneo yake ya kufanya kazi tofauti na mwenzake.
  • Jinsi ya kuandaa bajeti kwa MFUMO wa MTF
  • Maandalizi haya hufanywa na kila idara chini ya usimamizi wa idara mama ya Mipango na Takwimu. Kila idara lazima iwe na Mhusika mkuu wa maswala ya bajet
  • Taratibu za kuomba VAT Exemption
  • Taratibu za kuomba Msamaha wa kodi ya VAT. Kwanza inatakiwa kuwepo na barua ya Katibu mkuu wa Wizara ya Fedha kwenda kwa katibu Mkuu wa wizara ya  Maji ikionyesha kuridhiwa kwa kutolewa kwa Msamaha wa Kodi. Pia kunakuwepo na MOU kati ya wizara ya Maji, Fedha na Mipango pamoja na wafadhaili ambapo wadau wote tajwa wametia saini zao kuridhia MOU hiyo. Hivi vinaambatanishwa na Fomu maalumu ya kutoka TRA kwa ajili nya kuomba Msamaha wa kodi. Pia Katibu Tawala wa wilaya anatakiwa kuandika barua TRA ya kuthibitisha kuwa Mtoa huduma tajwa ana Mkataba wa kazi na WIlaya ya Tandahimba. Pamoja na hivyo vyote mktaba wa kazi tajwa inayoombewa Msamaha wa kodi unaambatanishwa.
  • Utaratibu wa kusimamia ujenzi wa miradi mikubwa na midogo
  • Usimamizi wa Miradi ya Maji hufanywa kwa njia mbili, Usimamizi kwa njia ya wafadhili na usimamizi kwa njia ya halmashauri na mkoa. Miradi isiyozidi bilioni moja itasimamiwa na halmashauri na miradi inayozidi bilioni moja itasimamiwa na wafadhali     

2.5 Chapisho la Sheria na Taratibu za usanifu mradi (MOWI designing Manual 2007)

2.6 Zabuni zinazoendelea kutekelezwa Idara ya Maji Mwaka 2016/2017

  • Ukarabti wa mradi wa maji vijiji vya Jangwani, Maheha, Umoja, Mundamkulu na Chipyai
  • Ukarabati wa mradi wa maji katika vijiji vya Litehu, Libobe, Liponde na Mkolachini
  • Ujenzi na Ukarabati wa mradi wa maji Mahuta
  • Ujenzi wa mradi wa maji Mkupete

2.11 Kazi muhimu/Nyeti   za Uhai wa Idara

  • Ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya maji
  • Uundaji na Usajili wa vyombo vya watumia maji (COWSOs)
  • Kusimaamia shughuli za uendeshaji na matengenezo ya miradi ya maji

Miradi

4.1 Miradi iliyotengewa fedha 2016/2017

  • Ujenzi wa mradi wa maji Mkwiti (vijiji vya mkwiti juu, Nannnala, Nanjanga, Ngunja, Mabeti, Chidede, Mkwitichini)
  • Ukarabati wa miundombinu ya maji Tandahimba mjini

4.2 Miradi inayotekelezwa

Jina la Mrdi
Kazi zilizopangwa kufanywa
Jina la Mkandarasi anayetekeleza
Ghrama za mkataba

Mradi wa maji Jangwani, Maheha, Umoja, Mundamkulu na Chipyai

Eker Co.Ltd


mradi wa maji katika vijiji vya Litehu, Libobe, Liponde na Mkolachini

Hecle Co.Ltd


Mradi wa Maji Mkupete

Reni Internation Co.Ltd


Mradi wa Maji Mahuta

Matrix Technology Co.Ltd


11.FEDHA NA BIASHARA

UTANGULIZI

Idara ya fedha ni miongoni mwa idara zilizopo katika halmashauri ya wilaya ya Tandahimba, idara inatelekeza majukumu yafuatayo katika utendaji kazi katika wilaya ya Tandahimba.

  • Kuandaa Bajeti ya mapato na matumizi ya mwaka mzima kwa kushirikiana na afisa mipango (w) na wakuu wengine wa Idara.
  • Kuhakikisha uwepo wa mfumo mzuri wa kihasibu na utunzwaji salama wa kumbukumbu za fedha za halmashauri.
  • halisi ukilinganisha na makisio ya Makusanyo na matumizi yaliyotengwa
  • Kuhakikisha usimamizi wa ndani wa fedha ni imara na unafanya kazi kulingana na taratibu na miongozo ya fedha.
  • Kuishauri halmashauri kuhusiana na masuala yote ya fedha.
  • Kuandaa taarifa za fedha ambazo zitaonyesha Makusanyo na matumizi
  • Kuandaa tarifa ya baraza na hesabu za Halmashauri za kila mwaka
  • Kuwasilisha taarifa na taratibu za kifedha katika kamati ya fedha kwa ajili ya kupata idhini na kuzigawanya kwa wakuu wengine wa idara.
  • Kutunza Mali zote za Halmashauri pamoja na mambo yote yanayohusiana na fedha za Halmashauri ukiwemo usimamizi na mpangilio bora wa watumishi katika utendaji kazi ndani ya idara ya fedha.

 

12.IDARA YA UJENZI

Majukumu ya Idara ya Ujenzi

Kitengo cha Majengo

  1. Kusimamia ujenzi/ukarabatu wa miundombinu ya majengo ya Shule za msingi na Sekondari
  2. Kufanya ujenzi/ukarabati wa miundombinu ya majengo ya yote ya halmashauri mfano. Zahanati, Vituo vya Afya na ujenzi wa Hospitali ya Wilaya.
  3. Kusimamia ujenzi/ukarabati wa kufanya ukaguzi wa majengo ya ofisi za vijiji, kata na majengo mengine yatakayohitajikakatika Idara za Serikali.
  4. Kupitisha vibali vya ujenzi na kufanya ukaguzi wa majengo hayo kwa mawasiliano na mhusika hatua kwa hatua.

Kitengo cha Magari na mitambo

  1. Kufanya ukaguzi wa magari/pikipiki na mitambo ya Serikali kabla ya matengenezo.
  2. Kufanya matengenezo madogo madogo.
  3. Kufanya ukaguzi baada ya matengenezo.

VITENGO

1.Kitengo cha Ufugaji Nyuki

2.Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani

3.Kitengo cha Sheria

4.Kitengo cha Ugavi na manunuzi

5.Kitengo cha Uchaguzi

6.Kitengo cha Teknolojia, habari, mawasiliano na uhusiano

Kazi za kitengo

 1.  Kuweka mahusiano bora baina ya Halmashauri pamoja naUmma na wadau mbalimbali pamoja na kutoa elimu kwa Umma.

  2   Kupokea nakushughulikia malalamiko pamoja na kuratibu masuala ya kiitifaki ikiwemokupokea wageni.

   3. Usimamizi Wa Mifumo Ya Kompyuta(System Administration)eneo hili linashughulikia usimamizi na uendeshaji wa mifumo yote ya kompyutakatika Halmashauri

5.  Usimamizi Wa Mtandao Wa Kompyuta Pamoja Na Vifaa Vyake(Network And Hardware Adminstration).

6.  Usimamizi Wa Benki Ya Takwimu(Database Administration) 

7.  Usimamizi wa tovuti na barua pepe (website administration & emails). 

8.Kutoa msaada wa kitaalamu kwa watumiaji wa mifumo ya kompyuta


Matangazo

  • Ratiba ya Usafi kila jumamosi ya mwisho wa mwezi. January 03, 2018
  • Siku ya mazoezi kila jumamosi ya pili ya mwezi January 03, 2018
  • TANGAZO LA UJIO WA MWENGE WA UHURU 2018 WILAYANI TANDAHIMBA June 09, 2018
  • Soma

Habari mpya

  • Kamati ya Fedha yaridhishwa na miradi ya maendeleo Halmashauri ya Tandahimba

    January 23, 2021
  • Kampeni ya ondoa mapori ongeza uzalishaji yashika kasi Tandahimba

    January 23, 2021
  • TEA yakabidhi miradi kwa Halmashauri ya Tandahimba

    January 19, 2021
  • Halmashauri ya Tandahimba yatumia shilingi Milioni 145 kutengeneza samani za kidato cha kwanza

    January 07, 2021
  • Soma

Video

Byakanwa Afunga mwaka kwa mikakati ya mabadiliko
Video nyingin

Kurasa za karibu

  • Ijue Tandahimba.

Viungio vinavyousiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • President's Official Website
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya sehemu

Tandahimba District Council

Wasiliana Nasi

    TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA

    Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA

    Simu: +25523 2410030

    Simu:

    Barua pepe: ded@tandahimba.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa