• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
Tandahimba District Council
Tandahimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Idara na Vitengo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Kumuona Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoko kwenye Mpango
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Zabuni
    • Kanuni na Taratifbu
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha habari
    • Habari Mpya
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya picha

Rc Byakanwa : ondoeni mikorosho iliyozeeka tuongeze uzalishaji

Posted on: December 10th, 2020

Na Kitengo cha Habari na Mawasiliano

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwa  amewataka wakulima Wilayani Tandahimba kuondoa mikorosho iliyozeeka na kupanda mikorosho mipya ili kuongeza uzalishaji wa zao hilo

Ameyasema hayo  kwenye ziara yake ya kampeni ya ondoa mapori ongeza uzalishaji Wilayani Tandahimba ambapo ametembelea mashamba  kata ya Chingungwe, Luagala na Mkoreha na kusitiza kuendelea kulima mazao mengine yanayokubali katika maeneo husika

Rc Byakanwa akionyesha Mikorosho iliyozeeka ambayo haiwezi kuzalisha ipasavyo

“ Tandahimba ni Wilaya inayoongoza kwa uzalishaji hapa nchini na wanunuzi wa Kimataifa wanajua hivyo lakini  uzalishaji unapungua kwakuwa mikorosho iliyopo mingi imezeeka ,na hakuna mapori mengi yaliyotelekezwa ila tatizo la hapa ni  mikorosho ya siku nyingi haina nguvu ya kuzalisha ipasavyo kwahiyo tuiondoe tupande mbegu bora”amesema Rc Byakanwa

 

Rc Byakanwa akisistiza  wananchi kubadilika  ili kuongeza uzalishaji wa zao la korosho

Aidha akitoa takwimu ya  uzalishaji  Wilaya ya Tandahimba kwa wananchi  amesema mwaka 215/2016  ilizalisha tani 40,000,mwaka 2016/2017 tani 70,000,mwaka2017/2018 tani 74,000,mwaka 2018/2019 tani 37,000,mwaka 2019/2020  tani 37,000 na msimu unaoendelea  tani 25000 hadi sasa zimeuzwa

 

Dc Sebastian Waryuba akitoa neno kwa wananchi wa kijiji cha Kuchele kata ya Chingungwe

Naye Mbunge wa Jimbo la Tandahimba Mheshimiwa  Katani Ahmad Katani  (CCM) amesema anaunga  mkono kampeni hiyo na atahakikisha wananchi wa Jimbo hilo hususani wakulima wanafuata kanuni za kitaalamu kwa kuondoa  mikorosho iliyozeeka na kupanda mipya  kwakuwa zao hilo ni uchumi wa wananchi wa Tandahimba

 

Mheshimiwa Katani(Mb) akimpongeza RC kwa kuanzisha kampeni hiyo ili kukuza uzalishaji wa zao la korosho

“Nakushukuru  Rc kwa kuja na kampeni hii mimi nitashirikiana na viongozi wa Wilaya kusimamia hili kwa wakulima wetu kuweza kuondoa  mikorosho ambayo imezeeka na kupanda mikorosho ya kisasa ili kuongeza uzalishaji,”amesema Mheshimiwa Katani

 


Pichani kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji (W)Said Msomoka ,wakuu wa Idara na Maafisa Tarafa ambao waliambatana na Rc katika ziara hiyo

Hata hivyo baada ya ziara hiyo wananchi katika maeneo hayo wameonyesha kuhamasika na kampeni hiyo na wataalamu kutoka Kituo cha Utafiti cha Naliendele na Bodi ya korosho Tanzania wameahidi kutoa ushirikiano  kwa wakulima ili kuongeza uzalishaji

 

Wananchi wakishuhudia jinsi ya ukataji sahihi wa mikorosho ili iweze kubebeshwa mbegu mpya kutoka kwa mtaalam kutoka kituo cha utafiti Naliendele

  


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 05, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI November 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MKATABA January 08, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MKIMBIZA MWENGE KIWILAYA March 30, 2024
  • Soma

Habari mpya

  • DC MNTENJELE AKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO SEKTA YA ELIMU

    June 25, 2025
  • DED MWANZALIMA ATEMBELEA MIRADI YA ELIMU

    June 21, 2025
  • TANDAHIMBA YAPATA HATI SAFI MARA YA TANO MFULULIZO.

    June 17, 2025
  • WAZIRI SIMBACHAWENE AMPONGEZA MKURUGENZI WA TANDAHIMBA NA MADIWANI KWA KUFANYA ZIARA YA MAFUNZO SIMIYU.

    June 11, 2025
  • Soma

Video

MKUU WA WILAYA YA TANDAHIMBA PAMOJA NA MKURUGENZI WASHIRIKI UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAHEHA
Video nyingin

Kurasa za karibu

  • Ijue Tandahimba.

Viungio vinavyousiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • President's Official Website
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya sehemu

Tandahimba District Council

Wasiliana Nasi

    TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA

    Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA

    Simu: +25523 2410030

    Simu:

    Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa