• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
Tandahimba District Council
Tandahimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Idara na Vitengo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Kumuona Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoko kwenye Mpango
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Zabuni
    • Kanuni na Taratifbu
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha habari
    • Habari Mpya
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya picha

Mkurugenzi Mtendaji akabidhi vifaa kwa shule maalum Mjimpya

Posted on: October 19th, 2020

Na Kitengo cha Habari na Mawasiliano

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba Said Msomoka amekabidhi vifaa  vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 4 kwa shule ya watoto wenye mahitaji maalum Mjimpya

Miongoni  mwa vifaa ambavyo amekabidhi Mkurugenzi Mtendaji Said Msomoka

Akikabidhi vifaa hivyo  ambavyo ni magodoro ,televisheni mbili  na Redio shuleni hapo amesema kuwa anafahamu mahitaji ni mengi  lakini atajitahidi kupunguza changamoto ambazo zimeainishhwa na Mwalimu Mkuu wa shule hiyo

Mkurugenzi Mtendaji Said Msomka (katikati) akiwa pamoja maafisa Elimu (kushoto) na Mdau wa Elimu (kulia)

“Natamani msome  katika mazingira mazuri zaidi kama mpo ulaya  lakini rasiliamali zetu ni chache hata hivyo tutashughulikia changamoto hizi kwa msimu  huu namuagiza Afisa Mipango ahakikishe tunamaliza changamoto hizi kama mabati kuvuja,ukosefu wa viti ili tuziwahi mvua ,”amesema Msomoka

Wanafunzi wakibeba magodoro hayo baada ya makabidhiano

Naye Kaimu Afisa Elimu  Msingi Martha Sinkamba amesema kuwa wazazi walete watoto wenye ulemavu wa akili katika shule hiyo  waweze kupewa ujuzi na elimu ili waweze kujisaidia wenyewe katika shughuli zao mbali mbali za kila siku

Mwalimu Mkuu(kushoto) akitoa shukrani kwa Kaimu Afisa Elimu Msingi Martha Sinkamba(kulia)

Naye Mdau wa Elimu Dorice Jeremiah ameweza kutoa magodoro 8 kwa ajili ya watoto hao”Mimi pia ni mzazi nimeguswa kuleta magodoro haya baada ya kupata taarifa kuwa wana uhitaji wa magodoro yaliyokuwepo ni chakavu,  natoa wito kwa wananchi na wadau wengine kuwasaidia watoto wetu wenye mahitaji maalum,”amesema Jeremiah

 

Mdau wa Elimu Dorice Jeremiah akizungumza na wanafunzi wenye mahitaji maalum

Aidha Mwalimu Mkuu wa shule maalum Mjimpya Karim Chipuputa amesema hadi sasa shule ina wanafunzi 80  wavulana 40 na wasichana 40 hivyo ameishukuru serikali kwa vifaa hivyo na mdau ambaye ametoa magodoro 8

Mkurugenzi Mtendaji Said Msomoka(kushoto)akipokea risala kutoka kwa mwalimu mkuu Karim Chipuputa(Kulia)

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 05, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI November 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MKATABA January 08, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MKIMBIZA MWENGE KIWILAYA March 30, 2024
  • Soma

Habari mpya

  • DC MNTENJELE AKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO SEKTA YA ELIMU

    June 25, 2025
  • DED MWANZALIMA ATEMBELEA MIRADI YA ELIMU

    June 21, 2025
  • TANDAHIMBA YAPATA HATI SAFI MARA YA TANO MFULULIZO.

    June 17, 2025
  • WAZIRI SIMBACHAWENE AMPONGEZA MKURUGENZI WA TANDAHIMBA NA MADIWANI KWA KUFANYA ZIARA YA MAFUNZO SIMIYU.

    June 11, 2025
  • Soma

Video

MKUU WA WILAYA YA TANDAHIMBA PAMOJA NA MKURUGENZI WASHIRIKI UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAHEHA
Video nyingin

Kurasa za karibu

  • Ijue Tandahimba.

Viungio vinavyousiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • President's Official Website
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya sehemu

Tandahimba District Council

Wasiliana Nasi

    TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA

    Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA

    Simu: +25523 2410030

    Simu:

    Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa