• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
Tandahimba District Council
Tandahimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Idara na Vitengo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Kumuona Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoko kwenye Mpango
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Zabuni
    • Kanuni na Taratifbu
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha habari
    • Habari Mpya
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya picha

Mwenyekiti Halmasahauri ya Tandahimba akabidhi viti na meza kwa ajili ya kidato cha kwanza 2021

Posted on: February 3rd, 2021

Na Kitengo cha Habari na Mawasiliano

Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba  imekabidhi viti na meza za wanafunzi  wa shule za sekondari kwa ajili ya kidato cha kwanza mwaka  2021 kwa Wakuu wa Shule za sekondari hatua ambayo imemaliza tatizo la ukosefu wa viti na meza kwa wanafunzi

Meza na viti vikishushwa kwenye gari kwa ajili ya makabidhiano

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Tandahimba ndugu Ally Machela amesema kuwa jukumu ambalo  wakuu wa shule wanapaswa kulizingatia ni  kuhakikisha wanaweka utaratibu kwa wanafunzi ambao wanatumia viti hivyo ili viweze kudumu

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Ally Machela akitoa neno kwa wakuu wa shule kwenye makabidhiano ya viti na meza

“Tumetumia kiasi kikubwa cha fedha za mapato ya ndani kwa ajili ya  kutengeneza samani hizi  jukumu kubwa mnalo  wakuu wa shule ni kuweka utaratibu ambao mwananfunzi atatunza kiti na meza atakazokabidhiwa,”amesema ndg Machela


Wakuu wa shule za sekondari wakisikiliza taarifa fupi ya ugawaji wa viti na meza hizo

Akikabidhi samani hizo  Mwewnyekiti wa Halamsahauri ya Wilaya ya Tandahimba Mheshimiwa Baisa Baisa amaesema kuwa Halmashauri imetimiza jukumu  la kutengeneza samani  ili wanafunzi wasome katika mazingira bora hivyo uwekwe utaratibu ili samani hizi zisiwe zinarudiwa kila mwaka kutengenezwa

Mwenyekiti Mh.Baisa Baisa akimkabidhi viti Mkuu wa shule ya sekondari Nandonde bi. Mboni Ahmad

“Nakabidhi samani hizi lakini wekeni utaratibu wa mwanafunzi kutunza samani zake,azitunze kuanzia anaanza kidato cha kwanza hadi anapomaliza  na endapo vitaharibika mzazi wake achukue hatua ya kutengeneza hii itasaidia kuwajenga wanafunzi wetu kuthamini na kutunza mali za umma,”amesema Mh. Baisa

Naye Mwenyekiti wa Walimu Wakuu wa Shule za Sekondari Tandahimba Ally Matangaru ameishukuru Halmashauri kwa jitihada wanazozifanya kwenye sekta ya Elimu na hivyo kuahidi  kuendelea kuweka juhudi kwenye kutoa elimu ili kuongeza ufaulu katika Halmashauri ya Tandahimba

Mh.Mwenyekiti  akimkabidhi meza Mwenyekiti wa Wakuu wa Shule ambaye pia  ni mkuu wa shule ya sekondari Namikupa

Aidha akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba  Katibu Tawala Juvenile Mwambi ameipongeza Halmashauri kwa jinsi ambavyo imefanikisha zoezi la ukamilishaji wa  samani hizo

Katibu  Tawala akitoa neno la pongezi kwa Halmasahauri kwa kukamilisha zoezi hilo

Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba imetoa kiasi cha zaidi ya Milioni 145 katika Mfuko wa Elimu kwa ajili  utengenezaji wa viti 2552 na meza 2492 ili kuondoa changamoto ya upungufu wa samani hizo kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza 2021

Matangazo

  • TANGAZO LA WALIOFAULU USAILI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. January 15, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI November 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MKATABA January 08, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MKIMBIZA MWENGE KIWILAYA March 30, 2024
  • Soma

Habari mpya

  • DC MNTENJELE AKABIDHI VISHIKWAMBI KWA MAAFISA UGANI TANDAHIMBA

    February 18, 2025
  • KU WILAYA YA TANDAHIMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU MWAKA 2025

    February 17, 2025
  • Vipaumbele Mahususi vya Bajeti ya 2025/2026 Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba.

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI TANDAHIMBA LAPITISHA MAKISIO YA MPANGO NA BAJETI YA TSH .BIL.40.2 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026.

    February 13, 2025
  • Soma

Video

MKUU WA WILAYA YA TANDAHIMBA PAMOJA NA MKURUGENZI WASHIRIKI UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAHEHA
Video nyingin

Kurasa za karibu

  • Ijue Tandahimba.

Viungio vinavyousiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • President's Official Website
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya sehemu

Tandahimba District Council

Wasiliana Nasi

    TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA

    Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA

    Simu: +25523 2410030

    Simu:

    Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa