Na Kitengo cha Mawasiliano
Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Tandahimba imeipongeza Halmashauri kwa utekelezaji wa Ujenzi wa vyumba kumi (10) vya madarasa kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha kwanza mwaka 2023
Akizungumza Januari 21,2023 katika ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa vyumba kumi vya madarasa mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Tandahimba Mhe.Ismaili Mkadimba amesema vyumba hivyo vimesaidia wanafunzi waliochaguliwa wote kuendelea na masomo
“Kamati ya Siasa tumekagua miradi hii ya ujenzi vyumba kumi vya madarasa tunaipongeza Halmashauri kwa kutekeleza miradi hiyo kwa wakati na wanafunzi wameanza kutumia,kikubwa tuendelee kuunga jitihada za Mhe.Rais wa awamu ya sita,anafanya kazi kubwa,anatekeleza sera za CCM kwa vitendo,”amesema Mhe.Mkadimba
Miradi iliyotembelewa na Kamati ya Siasa ni Ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa Shule yaSekindari Kwanyama,Ujenzi wa Vyumba vitatu shule ya Sekondari ya Mndumbwe na Ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa shule Sekondari ya Tandahimba
Aidha kiasi cha shilingi Milioni Mia mbili (200,000,000) zilitolewa na Serikali Kuu ambapo hadi kufikia Disemba 15,2022 miradi yote ilikamilika na wanafunzi wameanza masomo Januari 9,2023 katika madarasa hayo
TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA
Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA
Simu: +25523 2410030
Simu:
Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz
Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa