• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
Tandahimba District Council
Tandahimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Idara na Vitengo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Kumuona Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoko kwenye Mpango
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Zabuni
    • Kanuni na Taratifbu
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha habari
    • Habari Mpya
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya picha

Halmashauri ya Tandahimba yatoa Tsh. Mil 40 kukarabati vyumba viwili vya madarasa

Posted on: January 31st, 2021

Na Kitengo cha Habari na Mawasilinao

Halmashauri ya Tandahimba imetoa shilingi Milioni 40 kwa ajili ya ukarabati wa vyumba viwili vya madarasa  kwa shule ya Msingi Mkonjowano ambavyo vimeezuliwa na upepo  iliyoambatana na mvua na kusababisha wanafunzi 143 kukosa madarasa ya kusomea

Mkuu wa Wilaya akionyesha jinsi ofisi ya walimu ilivyoharibika  baada ya maafa hayo

Akizungumza kwenye eneo la tukio Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Sebastian Waryuba alimtaka Mkurugenzi kuharakisha  ukarabati wa majengo hayoa na kusistiza  kuendelea kupanda miti kwenye maeneo ya shule  kwasababu mvua huambatana  na upepo  mkali hivyo miti inasaidia kupunguza makali

Chumba cha  darasa la tatu , darasa la nne  na ofisi ya walimu inavyoonekana baada ya kuezuliwa na upepo

‘Uhalibifu huu  ni mkubwa lakini miti hii iliyopo imesaidia kupunguza makali ya upepo  kungekuwa hakuna miti kama hii athari ingekuwa kubwa zaidi kwaiyo endeleeni kuchukua tahadhari na mzingatie  kupanda miti mvua hizi zinapokuja zinaambatana na upepo mkali  sana kama maeneo hayana miti  maafa yanakuwa makubwa zaidi,”amesema Dc Waryuba

Dc Waryuba (kulia)akizungumza  na viongozi wa kata hiyo

Naye Kaimu Mkurugenzi Mtendaji ndugu Ally Machela baada ya kutembelea eneo hilo akiwa ameambatana na Afisa Elimu Msingi na Mwenyekiti wa Halmashauri walishuhudia  uharibifu ulifanyika katika shule hiyo

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Ally Machela

“Tumetembelea  tukaona hali ilivyo  Halmashauri imetoa kiasi cha shilingi milioni 40 kwa ajili ya vyumba hivyo vya madarsa viweze kukarabatiwa kwa haraka ili wanafunzi waendelee na masomo  kwenye madarasa yao,tayari mafundi wameanza kazi,”amesema Ndg Machella

Mwenyekiti wa Halmashauri  Baisa Baisa (wapili kushoto) akiwa na Kaimu Mkurugenzi  Ally Machela(watatu kushoto) ,Afisa Elimu na waheshimiwa madiwani ambao walitembelea eneo hilo

Naye Afisa Elimu Msingi  Bi Hadija Mwinuka amesema kuwa kwa sasa wananfunzi hao wa darasa la tatu na nne ambao madarasa yao yameezuliwa wanaendelea na masomo kwenye madarasa mengine  huku utaratibu wa kuharakisha ujekarabati wa madarasa yao unaendelea

“Madarasa ambayo yameezuliwa ni darasa la tatu na la nne lakini wanaendelea na masomo tulichofanya ni wanafunzi wa darasa la kwanza  na la pili wanaingia kwa kubadilishana wengine asb na wengine mchana 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA WALIOFAULU USAILI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. January 15, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI November 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MKATABA January 08, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MKIMBIZA MWENGE KIWILAYA March 30, 2024
  • Soma

Habari mpya

  • DC MNTENJELE AKABIDHI VISHIKWAMBI KWA MAAFISA UGANI TANDAHIMBA

    February 18, 2025
  • KU WILAYA YA TANDAHIMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU MWAKA 2025

    February 17, 2025
  • Vipaumbele Mahususi vya Bajeti ya 2025/2026 Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba.

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI TANDAHIMBA LAPITISHA MAKISIO YA MPANGO NA BAJETI YA TSH .BIL.40.2 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026.

    February 13, 2025
  • Soma

Video

MKUU WA WILAYA YA TANDAHIMBA PAMOJA NA MKURUGENZI WASHIRIKI UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAHEHA
Video nyingin

Kurasa za karibu

  • Ijue Tandahimba.

Viungio vinavyousiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • President's Official Website
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya sehemu

Tandahimba District Council

Wasiliana Nasi

    TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA

    Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA

    Simu: +25523 2410030

    Simu:

    Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa