• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
Tandahimba District Council
Tandahimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Idara na Vitengo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Kumuona Mh. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Kuonana na Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyoko kwenye Mpango
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Zabuni
    • Kanuni na Taratifbu
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha habari
    • Habari Mpya
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Video
    • Maktaba ya picha

Halmashauri ya Tandahimba yapongezwa ujenzi wa ofisi 41 za walimu

Posted on: January 22nd, 2022

Na Kitengo cha Habari na Mawasiliano

Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Mtwara imeipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba kwa ujenzi wa ofisi 41 za walimu

Shule shikizi Amani  iliyopo kata ya chaume

Mbunge wa Jimbo la Tandahimba Mhe.Katani Katani akieleza kwa kamati ya siasa jinsi shule shikizi zinavyowasaidia watoto wanatembea umbali mrefu

Pongezi hizo zimetolewa na Kamati ya siasa  Januari 21,2022 ilipotembelea utekelezaji wa miradi ya maendeleo ndani ya Halmashauri ya Tandahimba,Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mtwara ndugu Yusuf Nannila amesema jukumu liliopo ni wanafunzi  kuhakikisha wanaongeza bidii kwenye masomo ili kuongeza ufaulu katika Wilaya na Mkoa kwa ujumla

Kamati ya siasa ikitembelea miradi mbalimbali ya maendeleo

“Tumefanya ziara ya kutembelea miradi inayotekelezwa na ilani ya ccm,tunaipongeza Halmashauri ya Tandahimba kwa kumaliza miradi ya vyumba vya madarasa kwa wakati na  kujiongeza kwa kujenga ofisi 41 za walimu ambazo zitawasaidia walimu kukaa katika mazingira bora,nawapongeza sana kwa hatua hii,”amesema Mwenyekiti

 

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mtwara ndugu Yusuf Nannila akieleza jambo kwa wananchi wa Mambamba  (hawapo pichani) kwenye kituo cha afya cha Mambamba

Aidha katika ziara hiyo kamati ya siasa ilitembelea miradi ya elimu,afya na barabara ambapo imeridhishwa na  utekelezwaji wake na kusistiza kuwa  pale ambapo yameonekana mapungufu madogo madogo yarekebishwe kwa wakati sambamba na hilo imeagiza wakandarasi wa ujenzi wa barabara  ya Natosa kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa wakati

 

Kamati ya siasa wakikagua ujenzi wa barabara ya Natosa inayojengwa kwa lami ikiwa inaendelea na ujenzi huo

 

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe.Brigadia Jenerali Marco Gaguti  ambaye alikuwa kwenye ziara hiyo amehimiza wananchi kuhakikisha wanafunzi wote wanakwenda shule na kuongeza bidii kwenye masomo yao

 

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe.Brig.Jen.Marco Gaguti akiwahimiza wananchi wa kata ya Chaume Halmashauri ya Tandahimba kuhusu elimu

“Mkoa wa Mtwara suala la elimu bado lipo chini,niwaombe wazazi na walezi kuhakikisha wanafunzi wanahudhuria shule ambazo tayari zimefunguliwa kuanzia Januari 17,2022 lakini pia waongeze bidii katika masomo ili waweze kufikia malengo yao,”amesema Rc

 

 

Wakuu wa Idara na Vitengo wakiwa kwenye majumuisho ya ziara ya kamati ya siasa Mkoa wa Mtwara katika ukumbi wa mikutano wa Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba

 

Aidha wanafunzi wa Wilaya ya Tandahimba wameishukuru serikali ya awamu ya sita kwa ujenzi wa vyumba vya madarasa 88 na kuahidi kuongeza bidii kwenye masomo yao ili waweze kufikia malengo yao

 

Wanafunzi wa sekondari ya Nandonde wakiwa darasani miongoni mwa madarasa saba yaliyojengwa katika shule hiyo

Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba ilipata kiasi cha shilingi Bil.1.76 fedha za mpango wa maendeleo kwa ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya uviko-19 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 88 vya madarasa ambapo  ilijiongeza kwa kujenga ofisi za walimu 41 ambazo zimekwenda sambamba na ujenzi wa vyumba hivyo vya madarasa

 

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Tandahimba ndugu Mussa Gama akifafanua  jambo kwa wajumbe wa kamati ya siasa Mkoa

 






Matangazo

  • TANGAZO LA WALIOFAULU USAILI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. January 15, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI November 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MKATABA January 08, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MKIMBIZA MWENGE KIWILAYA March 30, 2024
  • Soma

Habari mpya

  • DC MNTENJELE AKABIDHI VISHIKWAMBI KWA MAAFISA UGANI TANDAHIMBA

    February 18, 2025
  • KU WILAYA YA TANDAHIMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU MWAKA 2025

    February 17, 2025
  • Vipaumbele Mahususi vya Bajeti ya 2025/2026 Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba.

    February 13, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI TANDAHIMBA LAPITISHA MAKISIO YA MPANGO NA BAJETI YA TSH .BIL.40.2 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026.

    February 13, 2025
  • Soma

Video

MKUU WA WILAYA YA TANDAHIMBA PAMOJA NA MKURUGENZI WASHIRIKI UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAHEHA
Video nyingin

Kurasa za karibu

  • Ijue Tandahimba.

Viungio vinavyousiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • President's Official Website
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya sehemu

Tandahimba District Council

Wasiliana Nasi

    TANDAHIMBA DC,MTWARA TANZANIA

    Anuani ya posta: P.O.BOX 03 TANDAHIMBA

    Simu: +25523 2410030

    Simu:

    Barua pepe: ded@tandahimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki ©2017 Tandahimba DC. Haki zote zimehifadhiwa